Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: – Je, kuna mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Tarafa ya Kintinku Manyoni?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri. Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Uvinza?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Josephine Genzabuke, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunafahamu Uvinza ni Wilaya mpya na kama zilivyo Wilaya nyingine hazijawa na Vituo vya Polisi vya ngazi ya Wilaya. Nimpe matumaini Mheshimiwa Mbunge kwamba tumeanza ujenzi wa Vituo vya Polisi kwenye hizi Wilaya zote mpya kadri tunavyoendelea kupata bajeti tutaifikia Wilaya ya Uvinza ambayo tunatambua iko mpakani itapewa kipaumbele katika ujenzi huo. (Makofi)

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: – Je, kuna mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Tarafa ya Kintinku Manyoni?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nini mpango wa Serikali kuwasaidia wananchi wa Kata wa Kamwanga, Wilayani Longido Mkoa wa Arusha, kumalizia Kituo cha Polisi ambacho walianza kukijenga kwa juhudu zao wenyewe?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine Magige, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza tuwapongeze wananchi ambao wamejitokeza kujenga Kituo cha Polisi huko Longido, niuelekeze Uongozi wa Polisi, Mkoa wa Arusha waweze kufuatilia kufanya tathmini kituo hicho kimefikia hatua gani na kinahitaji kiasi gani cha fedha ili kukamilisha ili tuweze kuingiza kwenye mpango wetu kutegemea upatikanaji wa fedha. Hilo jambo likishafanyika, basi tutakamilisha kituo hicho.

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: – Je, kuna mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Tarafa ya Kintinku Manyoni?

Supplementary Question 3

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba tulipitisha bajeti ya Bilioni Moja na Milioni Mia moja kwa ajili ya kujenga Kituo cha Polisi pale Ikungi na leo ni mwezi wa Novemba. Je, ni lini sasa Serikali italeta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho kama bajeti ilivyopitishwa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtaturu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba bajeti hiyo ilipitishwa kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho kinachofanyika ni Jeshi la Polisi limewasilisha mpango wa ujenzi ambao utakapopitishwa na Wizara utawasilishwa Hazina kwa ajili ya kutoa fedha. Ni matarajio yetu fedha za maendeleo kwa ajili ya ujenzi wa kituo hiki kwa vile zinatoka kwenye Mfuko ambao tunauzungumzia kwa ukamilifu wiki iliyopita zitatoka kwa ajili ya kuwezesha ujenzi wa kituo hicho kuanza. Ninaashukuru. (Makofi)

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: – Je, kuna mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Tarafa ya Kintinku Manyoni?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nashukuru sana kwa majibu mazuri kwa Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa tayari wananchi wa Tarafa ya Kintinku wameshatenga eneo la zaidi ya hekari nne katika Kijiji cha Lusilile kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi. Je, Naibu Waziri yuko tayari kuambatana nami kwa ajili ya kuona hilo eneo kama linafaa kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi?

Mheshimwa Spika, swali la pili; katika Makao Makuu ya Polisi ya Wilaya ya Manyoni, tuna upungufu mkubwa sana wa nyumba za watumishi hususani OCD na Mpelelezi wa Wilaya.

Je, nini commitment ya Serikali kuhakikisha kwamba tunawajengea watumishi hawa nyumba za kuishi? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Chaya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza niwapongeze wananchi wa Tarafa ya Kintinku kutenga hizo hekari nne ili kujenga Kituo chao cha Polisi, nami nitaungana na Mheshimiwa Mbunge wakati wowote atakapokuwa tayari kwenda kujiridhisha juu ya kituo hicho. Hata hivyo, hata kabla mimi sijaenda, niutake Uongozi wa Polisi Mkoa wa Singida waanze kutembelea eneo hilo na kama wanaona linafaa waweze kuwashauri ipasavyo wananchi hawa ili nitakapofika basi ni uamuzi uwe unafanyika.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili la ukosefu wa nyumba za watumishi akiwemo OCD Manyoni, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge, tumeripoti hapa wakati wa bajeti kwamba tunao mpango wa ujenzi wa vituo vya polisi na makazi ya askari na tutakwenda kujenga kwa awamu kwa kutegemea upatikanaji wa fedha. Ni matarajio yetu kabla ya mwaka 2025 Manyoni pia watakuwa mmefikiwa. Ahsante sana.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: – Je, kuna mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Tarafa ya Kintinku Manyoni?

Supplementary Question 5

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa fursa. Wananchi wa kata za Mbokomu na Uru-Shimbwe katika Jimbo la Moshi Vijijini wamejenga Vituo vya Polisi na bado havijakamilika.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi hawa waliotumia nguvu zao kujenga hivi vituo na kuwajengea nyumba Polisi wa Kata?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Prof. Patrick Ndakidemi, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze yeye na wananchi wake kwa kuanza ujenzi wa vituo hivi kwa kutumia nguvu zao na jitihada zao Mbokomu na Uru. Kama nilivyojibu kwenye swali lililoulizwa na moja ya Wabunge hapa tutawatuma Askari wetu upande wa Kilimanjaro ili wafanye assessment ya kiwango kilichofikiwa, kiasi gani kinatakiwa ili vituo hivi viweze kukamilishwa hatimaye tuviingize kwenye mpango wa ujenzi. Nashukuru. (Makofi)

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: – Je, kuna mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Tarafa ya Kintinku Manyoni?

Supplementary Question 6

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Hivi karibuni kumekuwa na wimbi la uhalifu katika Mikoa mbalimbali nchini. Je,Serikali ina mkakati gani wa kuunga mkono juhudi za wananchi nchi nzima ambao wameanzisha ujenzi wa Vituo vya Polisi ili kuweza kuvimalizia na hatimaye ulinzi uweze kuwa imara?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chaurembo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza uwepo wa wimbi la uhalifu ambao tumekuwa tukisema hapa uhalifu ni matokeo ya tabia na mwenedo wa jamii tunaupiga vita kwa nguvu zetu zote. Ndiyo maana yalivyojitokeza matukio haya ya panya road, ni jeshi halikulala hatimaye nchi imekuwa tulivu pia niwapongeze wananchi kwa kujenga Vituo vya Polisi mahala vinakohitajika ili mapolisi wawe karibu na wananchi.

Mheshimiwa Spika, kama nivyosema kwenye majiibu yangu ya msingi ya maswali yaliyopita, pale ambapo wananchi wamefanya kazi niwaombe Waheshimiwa Wabunge tuwasiliane na ma-OCD wetu na ma-RPC kwenye Mikoa yetu waweze kufanya tathmini kwenye kiwango cha ujenzi kilicho fikiwa na nini kinatakiwa kukamilisha, ili tuweze kuingiza kwenye mpango wa ugaramiaji kitaifa. Tukilifanya hilo itakuwa rahisi kuingizwa kwenye mipango. Nashukuru. (Makofi)

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: – Je, kuna mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Tarafa ya Kintinku Manyoni?

Supplementary Question 7

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ni lini sasa Serikali itaanzisha ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya katika Halmashauri ya Msalala?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, Mbunge wa Msalala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Msalala ni Wilaya mpya kama ilivyo Wilaya nyingine, tumeanzisha mpango wa ujenzi wa Vituo vya Polisi kwenye maeneo mapya ambayo hayakuwahi kuwa nayo, ni matarajio yetu kulingana na upatikanaji wa fedha Wilaya ya Msalala pia itafikiwa muda siyo mrefu ujao. Nashukuru. (Makofi)

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: – Je, kuna mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Tarafa ya Kintinku Manyoni?

Supplementary Question 8

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Hali ya Kituo cha Polisi cha Mchinga ambapo ndipo Makao Makuu ya Jimbo ni mbaya sana. Je, ni lini kitafanyiwa ukarabati Kituo hicho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salma Rashid Kikwete, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua Mchinga ndiyo Makao Makuu ya Jimbo na Wilaya. Niombe Mheshimiwa Mbunge uridhie nilishaahidi kufanya ziara katika Mkoa wa Lindi, moja ya maeneo nitakayopitia ni Mchinga ili kuona kiwango cha uchakavu wa kituo hiki tuweze kufanya mpango wa ukarabati ili kikamilike kiwe kituo stahiki kufaa kukaliwa na Askari wetu. Nashukuru. (Makofi)