Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 132 2022-11-10

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: –

Je, kuna mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Tarafa ya Kintinku Manyoni?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na Kituo cha Polisi pamoja na nyumba za makazi ya askari katika Tarafa ya Kintinku. Kwa sasa wakazi wa eneo hilo hupata huduma toka Kituo Kidogo cha Polisi kinachotumia jengo lililokuwa ghala la mazao ya kilimo waliloazimwa na Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni.

Mheshimiwa Spika, Serikali inamshauri Mheshimiwa Mbunge, ashirikiane na Uongozi wa Wilaya na Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, kutenga eneo mahsusi kwa ajili ya kujenga kituo na nyumba za askari ili Serikali iweze kukiingiza kituo hicho katika mpango wake na kukitengea fedha katika bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024.