Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya Mradi wa Maji wa Kiwira ili uanze kutekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Katika kipindi cha bajeti niliuliza swali la msingi kuhusiana na utekelezaji wa maji ya kutoka Mto Rufiji, nikaelezwa kwamba katika mwaka huu wa fedha wa 2022/2023, upembuzi yakinifu ungefanyika, sasa napenda kujua Serikali imefikia hatua gani katika upembuzi yakinifu uliotarajiwa? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Francis, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mto Rufiji ni moja ya mito muhimu sana kwa vyanzo vya maji ambavyo sisi tunavitumia. Tayari wataalam wetu wameshaanza kazi na tunatarajia watakamilisha upembuzi yakinifu kwa namna ambavyo muda umepangwa.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya Mradi wa Maji wa Kiwira ili uanze kutekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Napata shida sana mimi pamoja na wananchi wa Mkoa wa Mbeya, kwamba mradi wa zaidi karibu bilioni 300 sasa hivi unapewa shilingi 4,000,000,000, any way, ngoja niende kwenye maswali ya nyongeza.

Swali la kwanza; je, ni lini sasa Serikali itakamilisha mradi wa phase II ili kuhakikisha Wilaya ya Mbarali, Rungwe, Kyela na Chunya, Mbeya Mjini na Mbeya Vijijini ili waweze kupata maji?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Mheshimiwa Rais alivyokuja mwezi Agosti, 2022 alipita pale Wilayani Rungwe, alitoa agizo kwamba kufika mwezi Oktoba mradi wa maji unaoendelea pale Tukuyu uwe umekamilika, lakini sasa hivi Kata zote Bagamoyo, Msasani, Buliaga, Bitigi, Makandana, Kawetele maji ni shida kweli kweli. Sasa je, ni lini Serikali itakamilisha mradi huo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Suma Ikenda Fyandomo, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Suma Fyandomo amekuwa akifuatilia mradi huu muhimu, ni mradi wa kimkakati, phase II ambayo anaiulizia kupitia wilaya nyingine zote, itafanyika baada ya phase one kukamilika.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa hivi tayari kupitia Mhandisi Mshauri ameshamaliza kuandaa nyaraka za zabuni kwa kufikia tarehe 26 Oktoba, kupitia Mamlaka ya Maji na tayari Mamlaka ya Maji imetoa nyaraka za zabuni za kandarasi za ujenzi katika mradi huu na tunategemea kwa namna ambavyo wakandarasi wameshapatiwa tarehe 8 Novemba, kandarasi nne zimeshafanikiwa kufika kwenye eneo la mradi, kuangalia hali ya mradi ili sasa ifikapo tarehe 7 Disemba tunatarajia vitabu vya zabuni viwe vimetoka, kwa hiyo wataenda kuvichukua. Ikifika mwisho wa mwezi Disemba sasa hapo ujengaji wa mradi phase one ndio unaanza. Kwa hiyo kwa maeneo hayo aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge, yatafanyiwa kazi baada ya phase one kukamili.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na agizo la Mheshimiwa Rais, binafsi nilifika Tukuyu, nilikwenda kwenye chanzo, nilihakikisha tarehe ambayo tulimwahidi Mheshimiwa Rais, tuliweza kufikisha maji yale kutoka kwenye kile chanzo na tulishayaingiza kwenye existing line za Tukuyu Mjini na maji tayari yalishaanza kuingia kwenye maeneo yote. Kwa hiyo, kipindi hiki cha ukame, sio tu Tukuyu wala sio tu Mbeya, ni maeneo yote ya Tanzania tunapitia changamoto kwa sababu vyanzo vyetu vya maji kina kimeshuka.

Mheshimiwa Spika, kwa kupitia Bunge lako Tukufu, niombe sisi Wabunge wote tumwombe sana Mwenyezi Mungu mvua zinyeshe, hiyo ndio itakuwa suluhu na maeneo yote tutaendelea kupata maji kwa uzuri.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya Mradi wa Maji wa Kiwira ili uanze kutekelezwa?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwenye Mji wa Liwale upo mradi wa kuupatia maji mji ule na tumechimba visima vitatu Kijiji cha Turuki, lakini mradi ule sasa umesimama kwa muda mrefu. Je, lini hatima ya mradi ule ili Mji wa Liwale upate maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tulifika Liwale, mwenyewe nilikwenda Liwale, lakini vile vile Mheshimiwa Waziri amekwenda Liwale na huu mradi uliosimama, naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge nitaufuatilia leo hii na baada ya Bunge hili naomba tuonane.

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya Mradi wa Maji wa Kiwira ili uanze kutekelezwa?

Supplementary Question 4

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi. Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kwa kipindi hiki ina tatizo kubwa sana la maji. Naishukuru Serikali tuko katika Miji 28 lakini tunacho chanzo kizuri cha Ikorongo kwa kipindi hiki cha shida ya maji, Serikali inasema nini kwa kutu-support ukizingatia upembuzi yakinifu umeshafanyika? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sebastian Kapufi, Mbunge wa Mpanda Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa crisis ambayo tuko nayo sasa hivi ya ukame, vyanzo vyote ambavyo tunaviona bado vina maji mengi tunakwenda kuvitumia ili kuhakikisha tunakwenda kupunguza shida ya maji katika jamii zetu. Hivyo nitalichukua hili la chanzo cha Ikolongo na nitaagiza mara moja watu wetu ambao wako Mpanda kuhakikisha wanakifikia hiki chanzo na kuona kinatumika ipasavyo. (Makofi)

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya Mradi wa Maji wa Kiwira ili uanze kutekelezwa?

Supplementary Question 5

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa suluhisho pekee la kumaliza changamoto ya maji Wilaya na Nkasi, Mkoa wa Rukwa ni maji kutoka Ziwa Tanganyika. Ningependa kufahamu mchakato huo umefikia wapi wa kutoa maji Ziwa Tanganyika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, Mbunge wa Nkasi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, matumizi ya Ziwa Tanganyika yapo kwenye mkakati wa Wizara na tayari baadhi ya maeneo tumeshaanza kuyatumia maji ya Ziwa Tanganyika. Hivyo kwa maeneo ya Nkasi na maeneo yote ambayo yapo karibu na Ziwa Tanganyika, tunaomba waendelee kuvuta subira tutakwenda na tutahakikisha chanzo hiki cha uhakika tunakitumia.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya Mradi wa Maji wa Kiwira ili uanze kutekelezwa?

Supplementary Question 6

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Hali ya upatikanaji wa maji katika Kata ya Makanya, Kwekanga na Kwayi ni mbaya sana na ukizingatia sisi hatuna matatizo ya vyanzo vya maji. Je, ni lini Serikali itapeleka maji kwa haraka iwezekanavyo katika kata hizo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kata hizi alizozitaja pamoja na Makanya zipo kwenye utendaji wa kiwizara. Naomba nitumie Bunge lako Tukufu kumwarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba nitasimamia kuhakikisha ndani ya mwaka huu wa fedha haya maeneo yanapata maji.

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya Mradi wa Maji wa Kiwira ili uanze kutekelezwa?

Supplementary Question 7

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru kwa kunipa nafasi hii. Jimbo la Mtwara Mjini ni jimbo ambalo kidogo lina shida ya maji, lakini niishukuru Serikali kwa kutuletea bilioni 19 kwa ajili ya usambazaji wa maji kwenye Jimbo la Mtwara Mjini. Hata hivyo, tumechimba visima toka mwaka jana na vile visima vitatu mpaka sasa hivi havina mwelekeo wowote. Je, ni lini Serikali itamaliza visima hivi ili wananchi wapate maji kwenye Jimbo la Mtwara Mjini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nnaomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Mtenga, Mbunge wa Mtwara Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote nipende kupokea pongezi zake kwa Serikali kwa kazi kubwa ambayo imeshafanyika Mtwara. Kupitia visima hivi hata jana tumeongea na Mheshimiwa Mbunge, tayari nimeshawaagiza wale watendaji wetu pale Mtwara wanakwenda kulifanyia kazi na hili ni agizo la Mheshimiwa Waziri Mkuu, maeneo yote ambayo visima vilishachimbwa sasa hivi watendaji ni lazima kuvipa vipaumbele ili kuhakikisha vinasambaza maji kwenye maeneo yote ya wananchi.

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya Mradi wa Maji wa Kiwira ili uanze kutekelezwa?

Supplementary Question 8

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi. Je, ni lini Serikali itamalizia Mradi wa Bwawani katika Mji wa Karatu ili kukidhi uhitaji wa maji katika Mji wa Karatu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daniel Awack, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ameulizia kuhusu kumalizia mradi ambao tayari upo kwenye utekelezaji. Miradi hii tunapoianza inakuwa na ukomo wake, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutasimamia vizuri mradi ule ambao Mheshimiwa Waziri yeye mwenyewe ndio alifika pale na kutatua hii changamoto, hivyo tutasimamia kuhakikisha ndani ya muda wa mkataba mradi unakamilika.