Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 9 Water and Irrigation Wizara ya Maji 131 2022-11-10

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya Mradi wa Maji wa Kiwira ili uanze kutekelezwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Suma Ikenda Fyandomo Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha mapitio ya usanifu kwa ajili ya mradi utakaotumia chanzo cha Mto Kiwira kupeleka maji katika Jiji la Mbeya na Mji wa Mbalizi. Hatua inayoendelea sasa ni manunuzi ya Mkandarasi na katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga shilingi 4,000,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa chanzo na utekelezaji wa mradi utafanyika kwa awamu.