Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Salim Alaudin Hasham

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. ALAUDIN H. SALIM aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafungua barabara ya kimkakati inayotoka Mahenge mpaka Liwale kupitia Malinyi, Mlimba, Njombe na Songea?

Supplementary Question 1

MHE. ALAUDIN H. SALIM : Mhesnimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na kwamba Wilaya ya Ulanga ni kitovu cha uchimbaji wa madini, lakini pia kuna miradi mikubwa ambayo inaenda kuanza ya madini ya kinywa ambayo ina manufaa makubwa kwa nchi lakini pi kwa uchumi wa wananchi wa Wilaya ya Ulanga. Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kujenga barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 67 kwa kiwango cha lami?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Tarafa ya Mwaya ni tarafa inayoongoza kwa kilimo cha pamba pamoja na ufuta.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami ili wanachi hawa waweze kufikisha mazao yao sokoni kwa urahisi zaidi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika,naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Alaudini Hasham Salimu Mbunge wa ulanga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa Serikali ni kujenga barabara kwa kiwango cha lami. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa barabara ambazo zinarudiwa na TANROAD kutoka Mpilo – Mahenge iko kwenye mpango wa EPC+F na tayari Wakandarasi wameshapita na barabara aliyoitaja ya pili Serikali inaendelea kutafuta fedha ili iweze kuijenga kwa kiwango cha lami ili kurahisisha usafiri na kuwafanya wananchi wa Ulanga waweze kufanya biashara zao kwa urahisi. Ahsante.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ALAUDIN H. SALIM aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafungua barabara ya kimkakati inayotoka Mahenge mpaka Liwale kupitia Malinyi, Mlimba, Njombe na Songea?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua ni lini ujenzi wa kipande cha barabara kutoka Mbande - Kisewe mpaka Msongola utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chaurembo Mbunge wa Mbagala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja iko kwenye mpango na tunategemea utekelezaji utaanza mwaka huu wa bajeti.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. ALAUDIN H. SALIM aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafungua barabara ya kimkakati inayotoka Mahenge mpaka Liwale kupitia Malinyi, Mlimba, Njombe na Songea?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi, barabara ya USA River kwenda Oldonyo Sambu kwa kupitia Hifadhi ya Arusha imejengwa kwa kiwango cha lami hadi Getini Ngongongare.

Je, ni lini Serikali itaendelea na ujenzi wa barabara hii kutoka ngare na nyuki Kwenda Oldonyo Sambu na kuunganisha Barabara ya Kwenda Namanga na Moshi kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja ipo kwenye ilani na Mpango wa Serikali ni kuijenga kwa kiwango cha lami barabara aliyoitaja. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa jimbo lake kwamba Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kuijenga barabara hiyo.