Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 118 2022-11-09

Name

Salim Alaudin Hasham

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. ALAUDIN H. SALIM aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafungua barabara ya kimkakati inayotoka Mahenge mpaka Liwale kupitia Malinyi, Mlimba, Njombe na Songea?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Alaudin Hasham Salim, Mbunge wa Ulanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara inayotoka Mahenge kwenda Liwale ni Mahenge - Mwaya – Ilonga – Liwale ambapo sehemu ya Mahenge hadi Ilonga imefunguliwa na inapitika majira yote ya mwaka. Hata hivyo, kutoka Ilonga kwenda Liwale hakuna barabara kwa Mwalimu Nyerere na itahitaji kufanyiwa upembuzi yakinifu wa awali kuona iwapo inakidhi vigezo vya mazingira kabla ya kufunguliwa.