Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Primary Question

MHE. CHARLES J. MWIJAGE aliuliza: - Je, ni kwanini katika Tarafa ya Kamachumu mlalamikaji hulazimishwa kumgharamia mahabusu kwa kumsafirisha kwenda na kurudi rumande?

Supplementary Question 1

MHE. CHARLES J. MWIJAGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza: -

Mwaka jana Oktoba, Bibi yangu Ndugu Juliana Leo Gaesha, aliitwa kituo cha Polisi na kupelekwa Mahakama Kamachumu, Hakimu alimueleza mlalamikaji kwamba Bibi huyu apandishwe pikipiki na mlalamikaji akalipa fedha, Bibi yangu na watu wawili wakafungwa mshikaki kwenye pikipiki wakaenda Muleba, kufungwa Muleba magereza. Sasa kwa majibu yako Waziri ni lini mamlaka yako Wizara ya Mambo ya Ndani, Wizara ya Sheria na TAMISEMI, mtatengeneza Tume ya Kitaifa, yaani ngazi ya Taifa muende mpeleleze tukio hili la Juliana Gaesha? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa tukio hili lililotokea Muleba, kwa kweli hatuhitajiki kuunda Tume, badala yake wale ambao wako kule wanaosimamia utekelezaji wa sheria wazingatie sheria, labda kama jambo lingekuwa limepitiliza sana hiyo ipo haja ya kufanya hivyo. Lakini kwa kiwango hiki ninaamini wasaidizi wetu walioko ngazi hizo watazingatia na kuanza kutekeleza. Kama linaigusa Mahakama, wenzangu wa Mahakama wapo wamesikia litatekelezwa Mheshimiwa. Ahsante sana.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. CHARLES J. MWIJAGE aliuliza: - Je, ni kwanini katika Tarafa ya Kamachumu mlalamikaji hulazimishwa kumgharamia mahabusu kwa kumsafirisha kwenda na kurudi rumande?

Supplementary Question 2

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nina swali dogo tu. Kijiji cha Magungu wamejenga jengo la Kituo cha Polisi tangu mwaka 2016, nini kauli ya Serikali katika kuwasadia kumaliza lile jengo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mhesimiwa Olelekaita kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niwapongeze wananchi wa Kijiji hicho cha Magungu, kwa kufanya jitihada na juhudi kujenga Kituo cha Polisi. Tutakachofanya ni kufuatilia kiwango kilichofikia hilo jingo, linahitaji kiasi gani ili liweze kukamilishwa na tuone uwezekano wa kuingiza kwenye mpango wa ujenzi kutegemea upatikanaji wa fedha. Kama tulivyoongea juzi wakati wa ziara yangu nitafikia kwenye kituo hicho ili kuweza kuona hatua iliyofikia.(Makofi)

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. CHARLES J. MWIJAGE aliuliza: - Je, ni kwanini katika Tarafa ya Kamachumu mlalamikaji hulazimishwa kumgharamia mahabusu kwa kumsafirisha kwenda na kurudi rumande?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Je, ni lini Serikali itatoa fedha kuwasaidia wananchi wa Kata ya Mwika Kaskazini kumalizia kituo muhimu sana kwenye Soko Kuu la Mwika?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Kimei, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama wananchi wa Kata hiyo wameshajenga kituo wanahitaji kupata msaada wa Serikali kukamilisha tutahitaji tu uongozi wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro waweze kufanya tathmini kuona jengo limefika kiwango gani ili waweze kuliingiza kwenye mpango wa ujenzi kama tunavyofanya kwenye maeneo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Dkt. Kimei, tukupongeze kwa kuhamasisha wananchi na sisi tutakuunga mkono baada ya kupata uthamini huo.