Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 115 2022-11-09

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Primary Question

MHE. CHARLES J. MWIJAGE aliuliza: -

Je, ni kwanini katika Tarafa ya Kamachumu mlalamikaji hulazimishwa kumgharamia mahabusu kwa kumsafirisha kwenda na kurudi rumande?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Charles John Mwijage, Mbunge wa Muleba Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Polisi (Police Force and Auxiliary Service Act) Sura ya 322 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2002 na Kanuni 353 na 354 ya Kanuni ya Jeshi la Polisi (Police General Order) zinazosimamia watuhumiwa/mahabusu walioko kwenye Vituo vya Polisi, utaratibu wa kuwasafirisha watuhumiwa/mahabusu kwenda Mahakamani hutekelezwa na Jeshi la Polisi. Pia jukumu la kuwasafirisha watuhumiwa/mahabusu toka rumande Gerezani kwenda Mahakamani ni jukumu la Jeshi la Magereza kwa mujibu wa Kifungu cha 75 cha Sheria ya Magereza Sura ya 58 ya mwaka 1967 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2002.

Mheshimiwa Naibu Spika, kitendo cha mlalamikaji kulazimishwa kugharamia usafirishaji wa mtuhumiwa/mahabusu kwenda na kurudi rumande ni kukiuka Sheria na Kanuni zilizopo na kinatakiwa kuachwa mara moja. Wizara imefanya mawasiliano na Wakuu wa Vyombo vyetu, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) na Mkuu wa Jeshi la Magereza (CGP) ili wawaelekeze wasaidizi wao ngazi za Mikoa na Wilaya kuzingatia sheria hiyo. Ninashukuru.