Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, ni lini Vituo vya Afya vya Rukaragata na Nemba vitapewa vifaa vya upasuaji?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na hasa fedha ambazo zimetengwa kwa ajili ya kuhudumia vituo vya afya vilivyobaki. Kwa Kituo cha Nemba nashukuru kwa ajili ya vifaa vilivyopokelewa. Hata hivyo, nina swali moja la nyongeza; Kituo cha Afya cha Rukaragata ndicho kinachohudumia Wilaya ya Biharamulo Mjini, kwa sababu hatuna hospitali ya wilaya, kwa sababu hospitali iliyojengwa iko Kata jirani ya Lubungo. Sasa swali, kwa sababu tuna akinamama ambao wanajifungua pale na wanapata shida na hamna jengo la upasuaji na wametuambia tutapata pesa katika mwaka 2023/2024, ni mbali sana kwa sababu akinamama wanaendelea kuzaa na wanahitaji huduma. Sasa kwa sababu Waziri wa Fedha yuko hapa na Waziri ametuambia twende huko mbele, naamini Serikali inaweza ikapata fedha katika vyanzo vingine tukapata hii fedha katika mwaka huu wa fedha. Je, Waziri haoni haja ya kumpa nafasi Waziri wa Fedha aweze kutusaidia kwenye hili ili tuweze kupata fedha hii na akinamama wa Biharamulo waweze kunufaika na hili? Nashukuru.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge wa Biharamulo kwa swali lake na kwa kweli amekuwa akifuatilia sana wizarani fedha ya hospitali ya wilaya ambayo ni takribani milioni 204, pamoja na hili suala ambalo anasema hospitali yake ya wilaya, I mean kituo hiki cha mjini kinafanyika kama hospitali.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikuombe na nimwombe Mheshimiwa Mbunge aridhie tulichukue jambo hili Wizara ya Fedha ili tuwasiliane na wenzetu wa TAMISEMI, pamoja na yeye na Mkurugenzi wake, tuweze kuona namna ya kuliharakisha kwa ajili ya maisha ya Wanabiharamulo kama ambavyo amesema. (Makofi)