Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 109 2022-11-09

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: -

Je, ni lini Vituo vya Afya vya Rukaragata na Nemba vitapewa vifaa vya upasuaji?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Ezra John Chiwelesa, Mbunge wa Jimbo la Biharamulo Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2022/2023, imetenga shilingi bilioni 69.65 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma za afya kote nchini. Kati ya fedha hizo Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo imetengewa shilingi milioni 250.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imepeleka vifaa vya upasuaji ikiwemo kitanda, taa ya upasuaji na X-ray machine kwa ajili ya Kituo cha Afya Nemba.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Kituo cha Afya Rukaragata hakina jengo la upasuaji, Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo katika mwaka wa fedha 2023/2024, itatenga shilingi milioni 50 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa jengo hilo.