Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: - Je, nini mkakati wa Serikali kujenga chumba cha upasuaji kwa ajili ya Wajawazito katika Kituo cha Afya cha Itaka Wilayani Mbozi?

Supplementary Question 1

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Nimekuwa nikiuliza swali hili mara kwa mara na nishukuru sana Serikali kwa sababu imetupatia fedha kwa ajili ya ujenzi wa chumba cha upasuaji kwa ajili ya wanawake. Swali la kwanza; kwa kuwa Kituo hiki cha Afya cha Itaka kinatumika kama Kituo cha Afya cha Tarafa, kutokana na kwamba kata zote zinaunda Tarafa ya Itaka hazina vituo vya afya. Naomba kufahamu sasa ni lini Serikali itatupatia fedha kwa ajili ya ujenzi wa wodi za kawaida za watoto, wanaume pamoja na wanawake?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Sita, mama yetu Mama Samia Suluhu Hassan alipokuja kwenye kampeni mwaka 2020 katika Kata ya Mlowo…

NAIBU SPIKA: Uliza swali Mheshimiwa Shonza.

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Naibu Spika, sawa. Naomba kufahamu sasa, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake aliyoahidi Mheshimiwa Rais wa Awamu ya kutujengea kituo cha afya katika Kata ya Mlowo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Juliana Daniel Shonza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Mheshimiwa Shonza amekuwa akiulizia sana suala la Kituo cha Afya cha Itaka akishirikiana na Mheshimiwa Mbunge Mwenesongole, lakini nimhakikishie Serikali sikivu ya Awamu ya Sita, chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, imepeleka fedha hizo na kazi ya ujenzi wa jengo la upasuaji inaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie kwamba Serikali inajenga vituo vya afya hivi kwa awamu, tumeanza majengo hayo ya awali, lakini fedha itatafutwa kwenda kujenga wodi ya wanawake, watoto na wanaume.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na ahadi ya Mheshimiwa Rais, kujenga Kituo cha Afya katika Kata ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja, nimhakikisie kwamba ahadi za viongozi wetu ni kipaumbele. Kwa hiyo, Serikali tayari imeshaanza kufanya michakato ya kuhakikisha kwamba tunapata fedha kwa ajili ya kujenga kituo hicho cha afya. Ahsante.