Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza: - Je, ni Mikoa mingapi, Wilaya, Vijiji na Vitongoji wameunda Kamati za Watu wenye Ulemavu?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, naishukuru na kuipongeza Serikali kwa majibu yake mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa maeneo ambayo Kamati hizi zimekwishaundwa hazifanyi kazi kwa mujibu wa Sheria Na.9 ya Mwaka 2010. Je, ni sababu zipi zinazosababisha Kamati hizi kutokufanya kazi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; naipongeza pia Serikali kwa mikakati mizuri ambayo imewekwa kwa ajili ya ukamilishwaji wa kuundwa kwa Kamati hizi. Kutokana na umuhimu wa Kamati hizi na hasa ikizingatiwa kwamba zoezi hili limechukua muda mrefu kukamilika, je, ni lini Kamati hizi zitakamilika kuundwa?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stella Alex Ikupa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kuna baadhi ya maeneo ambapo Kamati hizi pamoja na kuundwa hazijawa na utekelezaji mzuri wa ufanyaji kazi. Changamoto hii siyo ya kisheria zaidi, sheria imeelekeza ziundwe na tayari zimekwishaundwa, changamoto iko katika eneo la kwanza ni elimu kwa wahusika wenyewe walio kwenye Kamati, lakini sehemu kubwa ni uwajibikaji wa wale ambao wamechaguliwa kuzihudumia Kamati hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la tatu ni usimamizi wa Kamati zenyewe. Jambo hili naomba nitumie Bunge lako Tukufu kwa niaba ya Waziri Mkuu kuwaomba na kuwaelekeza pia Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala, pamoja na Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya na Makatibu Tawala wa Wilaya waweze kusaidia na kusimamia utekelezaji wa sheria hii ili kuweza kuhakikisha inaleta ufanisi kama jinsi ilivyokusudiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili la nyongeza ameuliza kuhusu utekelezaji, kwamba lini tutakuwa tumekamilisha zoezi hili. Nieleze tu kwamba Serikali tunaendelea kufanya ufuatiliaji wa karibu kuweza kuhakikisha Kamati hizi zinafanya kazi effectively na wale ambao hawajaunda kupitia Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wahakikishe kwamba Kamati hizo zinaundwa na ufanisi upatikane.

Mheshimiwa Naibu Spika, itambulike kwamba suala la kutekeleza Sheria Na.9 ya Mwaka 2010 ya Watu Wenye Ulemavu sio suala la hiari, ni suala kisheria na ni la haki za binadamu.