Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 8 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 107 2022-11-09

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza: -

Je, ni Mikoa mingapi, Wilaya, Vijiji na Vitongoji wameunda Kamati za Watu wenye Ulemavu?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Ikupa Alex, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, uundwaji wa Kamati za Watu Wenye Ulemavu katika Ngazi ya Mkoa, Wilaya, Vijiji na Vitongoji ni kwa mujibu wa Sheria ya Watu Wenye Ulemavu Na.9 ya mwaka 2010 kifungu cha 14(1) ambacho kimeelezea juu ya uundwaji wa Kamati za Watu Wenye Ulemavu katika ngazi ya Kijiji, Mtaa, Wilaya, Mkoa pamoja na majukumu ya kila Kamati.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, imetekeleza kwa kiwango kikubwa uundwaji wa Kamati hizo. Mchanganuo wa idadi ya Mikoa, Halmashauri na Vijiji/Mitaa ya Tanzania Bara iliyounda Kamati za Watu wenye Ulemavu ni kama ifuatavyo: -

(i) Mikoa yote 26;

(ii) Halmashauri zote 185;

(iii) Vijiji 7,483 kati ya 12,319; na

(iv) Mitaa 2,284 kati ya 4,263.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha na kufuatilia Vijiji na Mitaa yote inaunda Kamati za Watu Wenye Ulemavu, Serikali imeandaa mikakati mbalimbali ikiwemo kuingiza masuala ya Kamati za Watu Wenye Ulemavu kwenye Mwongozo Kabambe wa Upangaji wa Mipango na Bajeti ya Huduma za Ustawi wa Jamii kwenye Halmashauri (Council Comprehensive Social Welfare Operation Plan – CCSWOP) ambapo utekelezaji wake utaanza mwaka ujao wa fedha 2023/2024. Aidha, Serikali itaendelea kufuatilia Watendaji wa Vijiji au Mitaa ili kuhakikisha Kamati za Watu Wenye Ulemavu zinaanzishwa katika maeneo yao.