Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga Kiwanja cha Ndege Singida Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Serikali lakini tangu 2017 mpaka sasa ni miaka mitano hakuna kinachoendelea. Swali la kwanza, nataka commitment ya Serikali lini ujenzi wa uwanja huo ama ukarabati utaanza?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, nataka kujua mkakati wa Serikali ambao utahakikisha ujenzi huu unafanyika kwa wakati? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ramadhan Sima, Mbunge wa Singida Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu katika jibu la msingi, ujenzi huu utaanza pale ambapo Serikali itakuwa imepata fedha na kuupangia uwanja huu kuanza ujenzi. Kwa hiyo, commitment ya Serikali ni kwamba tayari tumeshaanza hatua za awali kwa maana ya kufanya usanifu na kama nilivyoeleza kwenye jibu la msingi, tunaendelea kutafuta fedha pamoja na Washirika wa Maendeleo ili fedha ikipatikana tuanze kuujenga huu uwanja wa Singida.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga Kiwanja cha Ndege Singida Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Mkoa wa Manyara ambao eneo lilishatengwa eneo la Mwada?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sillo, Mbunge wa Babati Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, taratibu zinaendelea za kutwaa eneo ambalo uwanja huu utajengwa na baada ya taratibu hizo kukamilika uwanja huu utaanza kujengwa.