Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 99 2022-11-08

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga Kiwanja cha Ndege Singida Mjini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Ramadhani Sima, Mbunge wa Singida Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kiwanja cha Ndege cha Singida kilifanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ufadhili wa Benki ya Dunia mwaka 2017 kupitia mradi wa Transport Sector Support Project (TSSP) kwa ajili ya upanuzi na ukarabati wa Kiwanja hiki cha Ndege.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kutafuta fedha kutoka vyanzo vya Ndani na Washirika wa Maendeleo ili kuanza ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Singida.