Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Skimu za Umwagiliaji katika Jimbo la Mbogwe?

Supplementary Question 1

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kuuliza maswali mawili. Kwa kuwa mwaka 2021 tulipitisha bajeti kubwa na tukasema kwamba sasa mbegu zitatolewa na ruzuku, lakini mpaka sasa hivi mbogwe hatujaona kitu chochote. Majibu yake yakoje?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; nina imani hujawahi kufika katika Wilaya ile: Je, uko tayari kuongozana nami baada ya Bunge ili ukaangalie maeneo ya Mbogwe, maana ni maeneo yanayofaa sana kwa kilimo? Ahsante sana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nicodemas Henry Maganga, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la ruzuku la mazao hasa ya kimkakati yanaendelea kuratibiwa na bodi husika. Natoa maelekezo kwa bodi husika kuhakikisha kwamba wakulima wa pamba katika mikoa ambayo ameitaja Mheshimiwa Mbunge waweze pia kufikiwa na ruzuku hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, kuhusu mimi kwenda Mbogwe, baada ya kikao hiki cha Bunge, niko tayari kuongozana na Mheshimiwa Mbunge kwenda kuangalia suala la kilimo katika eneo lake la Mbogwe.

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Skimu za Umwagiliaji katika Jimbo la Mbogwe?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa nafasi hii. Serikali iliahidi kufanya ukarabati wa Skimu za Chikuyu na Udimaa: Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza ahadi hii? Ahsante sana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pius Chaya, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Skimu za Chikuyu na Udimaa ni skimu ambazo kama Naibu Waziri nimeshakwenda kuzitembelea, nimeziona na tumebaini changamoto yake. Ninavyozungumza hivi sasa, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Umwagiliaji na timu yake wanaelekea katika maeneo hayo kwa ajili ya kukamilisha kazi ya kupitia upya michoro na kuanza utekelezaji wa miradi ambayo itawafanya wananchi waendelee na kilimo cha umwagiliaji.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Skimu za Umwagiliaji katika Jimbo la Mbogwe?

Supplementary Question 3

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza; je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Skimu ya Kata ya Endagaw ilhali tayari ilishatoa zaidi ya shilingi milioni 800 na bado haijaanza kufanya kazi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asia Halamga, Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa wa Manyara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Skimu aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge ipo katika utekelezaji wa Bajeti ya mwaka huu, zoezi la utekelezaji linaendelea.