Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: - Je, Serikali inajua kwamba Zahanati ndogo ya Vunta iliyopo Kata ya Vunta kwenye Tarafa ya Mamba Vunta imewekwa bango la Kituo cha Afya cha Vunta badala ya Zahanati ya Kijiji cha Vunta?

Supplementary Question 1

MHE. ANNE K MALECELA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kupata nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nikiri kwamba sijaridhika na majibu ya Serikali. Kwa kuwa anavyoongea Waziri ni kama kweli Kata ya Vunta kuna kituo cha afya, lakini Kata ya Vunta kuna jengo ambalo Serikali ililirithi kutoka maendeleo ya jamii mwaka 1962 miaka 60 iliyopita. Je, Serikali katika hali ya namna hiyo, naomba uniambie Mheshimiwa Waziri, tena kiukweli, mna mpango gani wa kujenga kile Kituo cha Afya cha Kata ya Vunta?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Mheshimiwa Waziri Mkuu Ijumaa akimaliza kufunga Bunge hili mimi ninanyoosha, ninatangulia jimboni, wewe niambie unanifuata siku gani?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Anne Kilango Malecela kwa namna ambavyo anapambana kuhakikisha wananchi wa Jimbo la Same Mashariki wanapata maendeleo lakini pia huduma za afya. Nimhakikishie ni kwamba Serikali ilishafanya tathmini ya vituo vya afya vyote vyenye miundombinu pungufu ya kutoa huduma za afya. Tuna vituo vya afya ambavyo havina wodi na havina majengo ya upasuaji. Serikali tumeandaa database; na nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba Kituo cha Afya cha Vunta ni miongoni mwa vituo ambavyo tayari vimeingizwa kwenye database na vitatengewa fedha mwaka wa fedha 2023/2024 na tutapanua majengo yale ikiwemo kujenga jengo la upasuaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali hii sikivu ya Awamu ya Sita inafanya kazi hiyo na wananchi wa Same watapata huduma bora za afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusiana la kufuatana na yeye, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge niko tayari kuongozana naye ili twende moja kwa moja Same tukapite Vunta na kuweka mpango kazi wa utekelezaji wa mpango huu.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: - Je, Serikali inajua kwamba Zahanati ndogo ya Vunta iliyopo Kata ya Vunta kwenye Tarafa ya Mamba Vunta imewekwa bango la Kituo cha Afya cha Vunta badala ya Zahanati ya Kijiji cha Vunta?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru Mheshimiwa Naibu Waziri alifika Mbulu Vijijini na Mheshimiwa Waziri kwenye Kata ya Maga. Je, ni lini watatuletea fedha kwa ajili ya kujenga kituo cha afya katika Kata ya Maga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tumefanya ziara zaidi ya mara katika Jimbo hili la Mbulu, lakini nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri anayoifanya, na Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kumalizia vituo vya afya ambavyo havijakamilika.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa vituo vya afya vipya tuangalie utaratibu baada ya kukamilisha ujenzi wa vituo vya afya vya zamani lakini pia kupeleka vifaa tiba katika vituo hivyo.

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: - Je, Serikali inajua kwamba Zahanati ndogo ya Vunta iliyopo Kata ya Vunta kwenye Tarafa ya Mamba Vunta imewekwa bango la Kituo cha Afya cha Vunta badala ya Zahanati ya Kijiji cha Vunta?

Supplementary Question 3

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa nimeshawahi kuongea na Mheshimiwa Naibu Waziri mara kadhaa kuhusu kituo cha afya cha Une-Clinic Tabora, kwamba tunahitaji majengo ya upasuaji, theater na maabara ili kiweze kuwa kituo cha afya, kwa sasabu akina mama wajawazito wanazaa pale, kama akina mama 200 kwa mwezi.

Je, Serikali ni lini sasa itatuletea hizo fedha ili tuweze kukamilisha Kituo cha Afya cha Kaoni Clinic?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Munde, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mheshimiwa Munde amefuatlia suala Kituo cha Afya cha Town pale Tabora Manispaa; na alikuja pamoja na Mkurugenzi wa Manispaa, tulikubaliana wafanye tathmini ya ukubwa wa eneo lililopo ili tuweze ku-design michoro inayoweza kukaa pale ili tujenge jengo la ghorofa ili wananchi wa Tabora Manispaa wapate huduma.

Mhesimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nikuhakikishie kwamba zoezi hilo linaendelea litafanyiwa kazi na Serikali.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: - Je, Serikali inajua kwamba Zahanati ndogo ya Vunta iliyopo Kata ya Vunta kwenye Tarafa ya Mamba Vunta imewekwa bango la Kituo cha Afya cha Vunta badala ya Zahanati ya Kijiji cha Vunta?

Supplementary Question 4

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa na mimi nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Tabora Mjini lenye kata 29 ambalo ni kubwa sana kata nyingi za nje ambazo ni za vijijini zina upungufu mkubwa wa vituo vya afya, hasa katika Kata ya Uyui ambayo ina zahanati ambayo ingeweza Serikali ikaiboresha kuiweka kuwa kituo cha afya.

Je, Serikali inaahidi nini katika jambo hilo la kuzisaidia hizo kata za nje ya Mji wa Tabora?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Emmanuel Mwakasaka Mbunge wa Tabora Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika Manispaa ya Tabora kama ilivyo katika halmashauri zote kote nchini kuna upungufu wa vituo vya afya kwa baadhi ya kata. Dhamira ya Serikali ni kuhakikisha kwanza tunakamilisha ukamilishaji wa vituo vya afya vilivyoanza ujenzi na kupeleka vifaa vifaa tiba na watumishi ili vianze kutoa huduma za afya. Baada ya hapo tutafanya tathmini ya maeneo ambayo ni kimkakati kwa ajili ya kujenga vituo vya afya vingine ikiwemo katika eneo hili la Uyui.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.