Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 88 2022-11-08

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: -

Je, Serikali inajua kwamba Zahanati ndogo ya Vunta iliyopo Kata ya Vunta kwenye Tarafa ya Mamba Vunta imewekwa bango la Kituo cha Afya cha Vunta badala ya Zahanati ya Kijiji cha Vunta?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anne Kilango Malecela Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya Vunta kilichopo Tarafa ya Mamba Vunta ni miongoni mwa Vituo vya Afya sita vya Serikali vinavyotoa huduma kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Same. Kituo hicho kilipandishwa hadhi na kusajiliwa mwezi Januari, 2004 ambapo kilipewa msimbo namba 108286-6 na kinatambulika kitaifa kama Kituo cha Afya na si Zahanati.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Halmashauri ya Wilaya ya Same ilitenga Shilingi milioni 20 kupitia mapato ya ndani kwa ajili ya ukarabati wa jengo la maabara ambapo ukarabati huo upo katika hatua ya ukamilishaji. Aidha, katika Mwaka 2023/2024 Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Same itafanya ukarabati mkubwa wa Kituo cha Afya na kuongeza miundombinu ya huduma za upasuaji.