Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Abdulrahman Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Jimbo la Chambani?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa kuna vitendo vya uhalifu vinavyojitokeza katika Jimbo langu la Chambani, kama vile uwingizaji na utumiaji wa madawa, wizi wa mifugo na mazao.

Je, nili Serikali itaanza doria kwa kupambana na wahalifu hao?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abdulrahman Mwinyi Mohamed, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Abdulrhman Mwinyi kwa kujali utulivu usalama na amani kwenye Jimbo Lake la Chambani. Hata hivyo, kwa kuwa ujenzi wa vituo hivi utachukua muda nitoe maelekezo kwa RPC Mkoa wa Kusini Pemba kuimarisha doria kwenye maeneo korofi ambayo ni pamoja na Dodo, Chambani Pamoja na eneo la Chonga ili wenye vitendo vya wizi wa mifugo na mazao waweze kukoma. Ahsante.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Jimbo la Chambani?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa kituo cha Polisi Wilaya ya Itilima tayari umeshaanza na jengo limesimama, na Mheshimiwa Waziri kipindi kile alikuwa Naibu Waziri wa Fedha alikuja kutembelea, Waziri wa Mambo ya Ndani alikuja kutembelea.

Je, ni lini Serikali itatoa pesa za kumalizia ujenzi huo? Na Mheshimiwa Waziri nikuombe uje utembelee katika Wilaya yetu ya Itilima. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, natambua juhudi za wananchi wa Itilima pamoja na Mbunge wao Mheshimiwa Njalu Silanga katika kufuatilia ujenzi wa kituo hiki. Na kuhusu ombi lake, kwamba nitembelee Itilima, niko tayari kutembelea Itilima ili kuweka msukumo wa kupata fedha kutoka tunzo na tozo ili ukamilishaji wa kituo hiki uweze kufanyika.

Name

Simai Hassan Sadiki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nungwi

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Jimbo la Chambani?

Supplementary Question 3

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuweza kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la moja la nyongeza.

Ni lini Serikali itajenga uzio kuzunguka eneo la Kituo cha Polisi lilolokuwepo Nungwi ili kuepusha uvamizi eneo hilo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Simai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tutatathimini mahitaji ya gharama za ujenzi wa uzio huo ili kuweza kuanza mkakati wa ujenzi kupitia juhudi za mfuko wa tunzo na tozo kama ambavyo tumefanya kwenye maeneo mengine.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Jimbo la Chambani?

Supplementary Question 4

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Serikali imekuwa ikiahidi mara nyingi kujenga Kituo cha Polisi Itigi ambacho wanatumia majengo chakavu ya reli, angalau kituo cha daraja C. Sasa, je, ni lini?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Massare Mbunge wa Itigi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu uchakavu wa kituo kilichopo, tutafanya tathimini kuona kiwango cha uchakavu; na kama eneo hili halitoshi tuko tayari kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge ili eneo lipatikane la kutosha kwa ajili ya kujenga kituo chenye hadhi ya Wilaya ya Itigi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru.

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Jimbo la Chambani?

Supplementary Question 5

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Wananchi wa Kata ya Tula na Goweko wameanza ujenzi wa vituo vya afya. Ni lini Serikali itapeleka fedha kuungana na wananchi kumalizia vituo hivyo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Igalula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tutafanya tathimini ya kuangalia kiwango cha ujenzi uliofikiwa ili kuona kiasi cha fedha ambazo zinahitajika kumalizia ujenzi wa kituo hicho, na gharama zitakapojulikana zitajumuishwa kwenye mapango wetu wa umaliziaji wa vituo vya polisi vikiwemo hivyo vya Goweko na Igalula.

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Jimbo la Chambani?

Supplementary Question 6

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Naibu Spika, Neema Mwandabila.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mji wa Tunduma upo mpakani na kituo kilichopo pale hakina hadhi ya kuweza kuhudumia katika eneo lile; wahalifu ni wengi kiasi kwamba kinalemewa.

Ni lini Serikali itaona umuhimu wa kujenga kituo cha chenye hadhi ya Wilaya katika eneo la Tunduma?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema Mwandabila kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu hivi majuzi kwamba Wilaya zote ambazo hazina vituo vya polisi ni mpango wa wizara kuanza ujenzi kwenye maeneo hayo. Kwa hiyo, eneo analolitaja hili ni moja ya maeneo ambayo yatazingatiwa katika ujenzi wa vituo vya polisi.

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Jimbo la Chambani?

Supplementary Question 7

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niulize swali la nyongeza.

Ni lini Serikali itajenga kituo cha polisi cha Wilaya Uvinza?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu Wilaya ya Uvinza ni miongoni mwa wilaya mpya ambazo hazina vituo vya polisi, na kwa hiyo katika mkakati wetu wa kuhakikisha mikoa na wilaya zote ambazo hazina vituo vinajengewa vituo hivyo Uvinza ni eneo mojawapo litakalo zingatiwa katika ujenzi wa vituo vipya vya polisi.