Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 39 2022-04-11

Name

Mohamed Abdulrahman Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. MOHAMED ABDULRAHMAN MWINYI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Jimbo la Chambani?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abdulrhman Mwinyi Mohamed Mbunge wa Chambani kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Chambani liko katika Wilaya ya Mkoa wa Kusini Pemba. Wilaya hii ina vituo vya polisi vine ambavyo ni Mkoani, Kengeja, Mtambile, na Mkanyageni. Wananchi wa Chambani wanapata huduma ya polisi kwenye vituo vya Mtambile na Kengeja ambavyo viko ndani ya kilometa sita.

Kwa sasa Serikali kupitia Jeshi la Polisi linatarajia kujenga Vituo vya Polisi maeneo ya vitongoji, Pujini, Wesha na Gombani Wilayani Chakechake ambayo ina kituo kimoja tu cha Polisi katika mkoa wa Kusini Pemba.