Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mahenje - Ndolezi - Hasamba hadi Vwawa ambayo ni muhimu kwa utalii wa Kimondo cha Mbozi na usafirishaji wa mazao?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHAT N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa, eneo la Mlowo mpaka Vwawa kumekuwa na msongamano mkubwa sana wa magari na hasa malori ya mizigo yanayopitia pale Tunduma na kuelekea huku sehemu mbalimbali, na barabara hii ambayo tunaisema ya kuanzia Mahenje, Ndolezi, Hasamba inaweza ikangezewa upembuzi yakinifu katika eneo la Ilyika, kwenda kule Kilima Mpimbi mpaka hadi pale Iboya na ikawa ni bypass.

Je, Serikali iko tayari sasa kuongeza hicho kipande kilichobaki kwa ajili ya kufanya usanifu wa kina na kuhakikisha kwamba inakuwa ni bypass? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali pili, kwa kuwa sasa wanajenga hizo mita 800 mpaka hadi pale karibu na hospitali ya Mkoa wa Songwe.

Je, Serikali itakuwa tayari katika mwaka ujao wa bajeti huu ambao tunaujadili kutenga tena kiasi fulani cha fedha kwa ajili ya kujenga kutoka pale kwenda Hasamba mpaka Ndolezi kwenye kimondo ili kusudi watalii mbalimbali waweze kufika katika eneo la Kimondo?(Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Hasunga, Mbunge wa Vwawa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba barabara ya kutoka Mlowo hadi Tunduma kumekuwa na msongamano mkubwa wa magari. Kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, tunafanya usanifu kuanzia Mahenje, Hasamba hadi Vwawa, sasa swali alilolitoa la kutoka Mahenje Vwawa na kufanya bypass hadi Iboya ni barabara ambayo kimsingi kwa sasa haiku chini ya TANROAD lakini wazo hilo kwa maana ya kupunguza msongamano kupita Wilaya ya Vwawa, Serikali imelichukua na italiangalia namna ya kulifanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoisema ya kuendeleza ni utaratibu wa kuendelea na ndiyo maana tumesema tutakwenda kwa awamu. Kwa hiyo, tunauhakika kwamba katika bajeti inayokuja, baada ya kukamilisha hizo mita 800 tutaendelea na lengo ikiwa ni kukamilisha barabara zima ambayo sasa tunafanyia usanifu. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mahenje - Ndolezi - Hasamba hadi Vwawa ambayo ni muhimu kwa utalii wa Kimondo cha Mbozi na usafirishaji wa mazao?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami, barabara inayounganisha Mkoa wa Lindi na Mtwara, RuangWa – Nachingwea - Masasi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hokororo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni mpango wa Serikali kuijenga barabara ya Masasi -Nachingwea kwa kiwango cha lami, lakini itaanza tu pale ambapo Serikali itakuwa imeshapata fedha kwani tayari usanifu wa kina ulishakimilika, kwa hiyo kinachosubiriwa ni upatikana wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mahenje - Ndolezi - Hasamba hadi Vwawa ambayo ni muhimu kwa utalii wa Kimondo cha Mbozi na usafirishaji wa mazao?

Supplementary Question 3

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ujenzi wa barabara ya Loliondo - Mto wa Umbu, kipande cha Wasso - Sale umeshakamilika kwa kiwango cha lami. Nilitaka kufahamu, je, ni lini Serikali itaanza awamu ya pili ya ujenzi huu ambao ni Sale-Ngarisero.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii imekuwa kero sana kwa kazi wa Ngorongoro, hasa Tarafa ya Loliondo na Tarafa ya Sale. Kwa hiyo, Mheshimiwa Naibu Waziri anapokuja kunijibu naomba anipe la uhakika na linaloeleweka. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Magige, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ya Mto wa Umbu, Loliondo, Sale, hadi Wasso, kipande cha Sale Wasso kimeshakamilika na kipande cha Loliondo kuja Ngarisero kiko kwenye mpango wa kujengwa. Lengo ni kukamilisha barabara yote ambayo ni muhimu sana siyo tu kwa wananchi wa Loliondo lakini kwa shughuli pia za utalii.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mahenje - Ndolezi - Hasamba hadi Vwawa ambayo ni muhimu kwa utalii wa Kimondo cha Mbozi na usafirishaji wa mazao?

Supplementary Question 4

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na changamoto kubwa sana ya foleni pamoja na msongamano wa magari kuanzia eneo la Mpemba, Sogea mpaka unafika Custom Tunduma. Naomba kufahamu Serikali imejipangaje kutuondolea adha hiyo wananchi wa Mkoa wa Songwe kwa kutujengea barabara kutoka Mbozi, kwa maana ya pale Mlowo mpaka kufika Tunduma?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juliana Shonza, Mbunge wa Viti Maalum Songwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja ni sehemu tu ya barabara ya Igawa, Mbeya hadi Tunduma, maeneo yote haya yameshafanyiwa usanifu na yale maeneo ya Miji, barabara hizi zitajengwa njia nne ili kupunguza msongamano wa katika maeneo ya Miji ikiwemo na hilo eneo la kuanzia Vwawa kwenda sehemu ambapo tutajenga mizani.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mahenje - Ndolezi - Hasamba hadi Vwawa ambayo ni muhimu kwa utalii wa Kimondo cha Mbozi na usafirishaji wa mazao?

Supplementary Question 5

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa kutoka Mbagala Kokoto mpaka Kongowe ili kupisha ujenzi wa barabara hiyo ambayo umetengewa fedha katika mwaka huu wa fedha. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chaurembo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ya Kokoto kwenda Kongowe, hawa wananchi watalipwa fidia pale ambapo barabara hii itaanza kujengwa, ahsante.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mahenje - Ndolezi - Hasamba hadi Vwawa ambayo ni muhimu kwa utalii wa Kimondo cha Mbozi na usafirishaji wa mazao?

Supplementary Question 6

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Kwasadala - Kware - Lemira Kati, kilometa 15.2 ni barabara muhimu sana inayoshusha mazao kwenye soko la Kwasadala na hatimae kuja huku Dodoma na sisi kuweza kuitumia.

Je, Serikali ni lini itajenga barabara hii kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saasisha Mafuwe, Mbunge wa Hai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja ya Kware - Lemira ni barabara muhimu sana kwa wananchi wa Hai. Hivi tunavyoongea ni kwamba Serikali inatafuta fedha ili fedha ikipatikana barabara hii ambayo siyo ndefu iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mara Serikali itakapopata fedha barabara hii ambayo inasimamiwa na TANROADS itajengwa kwa kiwango cha lami. (Makofi)

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mahenje - Ndolezi - Hasamba hadi Vwawa ambayo ni muhimu kwa utalii wa Kimondo cha Mbozi na usafirishaji wa mazao?

Supplementary Question 7

MHE. DKT. JOHN D. PALLAGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona.

Je, ni lini Serikali itaendelea na ujenzi wa barabara ya njia nne kuanzia Tengeru kwenda Holili ambayo ni sehemu ya mradi wa barabara ya Afrika Mashariki unaoanzia Sakina. Barabara hii ujenzi wake ulisimama takribani sasa hivi miaka Minne.

Je, ni lini ujenzi utaendelea kwa sababu barabara ile sasa hivi ina magari mengi sana na ajali ni nyingi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pallangyo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli barabara hii inayotoka Arusha kwenda Holili ipo kwenye mpango, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari tunategemea mwaka wa fedha unaoanza kujenga kati ya Tengeru na Usa River, barabara nne, lakini daraja la Kitafu litajengwa na barabara za Moshi Mjini zitajengwa katika huu mpango. Ahsante.

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mahenje - Ndolezi - Hasamba hadi Vwawa ambayo ni muhimu kwa utalii wa Kimondo cha Mbozi na usafirishaji wa mazao?

Supplementary Question 8

MHE. BONNAH L. KAMOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri ni lini Serikali itakarabati daraja la Kimanga ambalo linazunguka Tabata, pamoja na Kata zingine? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Kamoli Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ukarabati wa barabara hii upo kwenye usanifu na mara usanifu utakapokamilika daraja hili litajengwa. Ahsante.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mahenje - Ndolezi - Hasamba hadi Vwawa ambayo ni muhimu kwa utalii wa Kimondo cha Mbozi na usafirishaji wa mazao?

Supplementary Question 9

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya kutoka Ilula, Mlafu, kuelekea Kilolo ni barabara ambayo ni mbaya sana. Ni lini itajengwa kwa kiwango cha lami kwa sababu wakulima wa kutoka Kilolo wanatataka kusafirisha mazao yao? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tendega Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli barabara aliyoitaja iko katika hali mbaya lakini ni azma ya Serikali kwamba kabla ya kuanza kuijenga itaikarabati kwanza ili iweze kupitika wakati Serikali ikitafuta fedha kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mahenje - Ndolezi - Hasamba hadi Vwawa ambayo ni muhimu kwa utalii wa Kimondo cha Mbozi na usafirishaji wa mazao?

Supplementary Question 10

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Liwale inazo barabara moja muhimu sana, barabara ya uchumi, barabara ya Mkombozi. Barabara hii nimeizungumza mara nyingi mno, barabara ya Nangurukuru Liwale. Wananchi wa Liwale wanataka kusikia barabara hii itajengwa lini kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ilishakamilishwa kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, Mheshimiwa Kuchauka atakubaliana nami kwamba Wizara ina mpango wa kuanza kuijenga barabara hii walau kwa awamu mwaka wa fedha unaokuja. Kwa hiyo, itategemea sana na upatikanaji wa fedha, lakini Serikali ina mpango kuianza kuijenga kwa kiwango cha lami.