Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 4 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 37 2022-04-11

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mahenje - Ndolezi - Hasamba hadi Vwawa ambayo ni muhimu kwa utalii wa Kimondo cha Mbozi na usafirishaji wa mazao?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Japhet Ngailonga Hasunga, Mbunge wa Vwawa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Songwe inajenga kwa kiwango cha lami barabara hii kwa awamu. Hadi mwishoni mwa Machi, 2022 Kilometa 4.5 zimekamilika kujengwa kuanzia Mji wa Vwawa hadi Kijiji cha Mtambwe katika hospitali ya Mkoa wa Songwe. Aidha, ujenzi unaendelea kwa sehemu ya mita 800 na inatarajiwa ifikapo mwishoni mwa Mwezi Juni, 2022 ujenzi utakuwa umekamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ya barabara hii iliyobaki kilomita 26.56 kwa sasa inafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na kampuni ya Mhandisi Mshauri M/S Inter Consult Ltd ya Dar es Salaam. Kazi hii inatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2022. Baada ya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami. Ahsante.