Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, ni Vyuo Vikuu vingapi vimepewa fursa ya kuajiri watumishi wake?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu hayo ya Waziri, naomba kufahamu kuhusu wale Maprofesa na Madaktari 203 ambao walistaafu kwa sasa wako wapi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, sehemu ambayo nguvu zinaisha haziwezi kufanya kazi ni sehemu ya ubongo. Kwa hiyo ina maana kwamba mtu anaweza akafanya kazi hata akiwa na miaka 70 mpaka 75 kama tunavyoona baadhi ya maprofesa humu ndani. Sasa ni lini Serikali kama Waziri alivyoahidi mwaka jana, ni lini Serikali sasa itaruhusu hawa watumishi wanaostaafu kwa miaka 65 waendelee kubaki chuoni mpaka miaka 75?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Ntara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Dkt. Ntara kwa kufuatilia kwa karibu sana maendeleo pamoja na upatikanaji wa watumishi hasa Wahadhiri katika vyuo vyetu. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ni kweli kulingana na miongozo ya Utumishi wa Umma, wenzetu katika vyuo vikuu, Wahadhiri wale pamoja na Maprofesa huwa wanastaafu wakifikia umri wa miaka 65, tofauti na maeneo mengine ya Utumishi wa Umma.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika kipindi cha miaka mitatu watumishi zaidi ya 203 walistaafu kwenye maeneo mbalimbali ya vyuo vyetu hapa nchini. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Dkt. Ntara kwamba miongoni hawa watumishi 203 ambao wamestaafu basi watumishi karibu 103 walikuwa wamebakishwa vyuoni kwa mikataba maalum. Miongoni mwao walikuwa ni watumishi 98 ambao walikuwa ni Maprofesa na watumishi karibu watano walikuwa ni Senior Lectures.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, ni Vyuo Vikuu vingapi vimepewa fursa ya kuajiri watumishi wake?

Supplementary Question 2

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Msalala ni miongoni mwa Halmashauri ambazo hazina Vyuo Vikuu na tayari kupitia mapato ya ndani tumetenga fedha kiasi cha Shilingi Milioni 212 kuanza ujenzi wa Chuo cha VETA. Sasa ni Serikali itatuongezea fedha ili tuweze kumaliza chuo hicho?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali katika sera yetu tunahakikisha kwamba tunakwenda kuwa na Vyuo vya VETA katika kila Wilaya nchini, kwa kuanzia tulianza na Wilaya 29 na hivi sasa vyuo hivyo vinakwenda kumalizika pamoja na Mikoa Minne ambayo haikuwa na Vyuo vya VETA. Nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mwaka wa fedha ujao, mambo mengi sana kulingana na upatikanaji wa bajeti vyuo hivi tutakwenda kujenga kwenye maeneo ambayo bado ujenzi haujafanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Name

Dr. Paulina Daniel Nahato

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, ni Vyuo Vikuu vingapi vimepewa fursa ya kuajiri watumishi wake?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. PAULINE D. NAHATO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Je, ni lini kutakuwa na usawa wa jinsia katika uongozi wa juu katika Vyuo vyetu Vikuu kwa sababu kwa sasa hivi katika Vyuo Vikuu hakuna usawa wa jinsia kwa uongozi, ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Dkt. Nahato kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tuna changamoto sana kwenye usawa wa jinsia kwenye level hiyo ya Vyuo Vikuu na hii ni kutokana tu kwamba wakati tunaendelea na masuala haya ya kusoma, wenzetu hawa wa jinsia ya kike huwa wana drop sana. Lakini nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge jambo hili sasa tunaenda kulizingatia katika taratibu za sasa hivi utumishi maeneo haya ya jinsia yanazingatiwa sana hasa katika mradi wetu ule wa HEET ambao nilizungumza katika kipindi kilichopita, zaidi ya Wahadhiri zaidi ya 600 tunaenda kuwasomesha na miongoni mwao tutaweka ajenda maalum kabisa katika kuhakikisha kwamba jinsia inaweza kuzingatiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana.(Makofi)