Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 4 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 36 2022-04-11

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: -

Je, ni Vyuo Vikuu vingapi vimepewa fursa ya kuajiri watumishi wake?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Thea Medard Ntara, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Vyuo Vikuu kama zilivyo taasisi nyingine za Umma huajiri watumishi baada ya kupata vibali vya ajira kutoka Wizara yenye dhamana na Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jumla ya Vyuo Vikuu vya Umma 13 kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita (2018-2019 mpaka 2020/2021) vilipata vibali vya kuajiri watumishi 618 ambapo wanataaluma ni 333 na waendeshaji ni 285.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na fursa hizo za kuajiri watumishi zilizotolewa, bado Serikali inaendelea na taratibu za kuwahamisha watumishi wenye sifa kutoka sehemu mbalimbali kujiunga na utumishi katika Vyuo Vikuu. Aidha, Serikali itaendelea kutoa vibali vya ajira katika Vyuo Vikuu kwa lengo la kuviongezea fursa ya kuajiri watumishi kadri ya upatikanaji wa fedha.