Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji Igando - Kijombe ili kupunguza changamoto ya maji Jimbo la Wanging’ombe?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante Mradi wa Maji Matamba - Kinyika wenye thamani ya bilioni mbili ndani ya miaka minne sasa Wilaya ya Makete bado haujakamilika. Naomba kujua, je, ni lini Serikali itasambaza mabomba pamoja na kujenga ofisi ili wananchi wa Wilaya ya Makete waweze kupata maji kwa uhakika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema William Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nipende kumpongeza Mheshimiwa Neema kwa ufuatiliaji mzuri wa miradi mbalimbali katika Mkoa wa Njombe. Kwa upande wa Makete nilifika huko na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo tulitembelea miradi hii yote na mradi huu ni kipaumbele cha Wizara kwa sababu unakwenda kuhudumia wananchi wengi na lengo la Serikali ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ni kuona maji yanapatikana katika maeneo yote. Maeneo ambayo muda mrefu hayajapata nayo yanakwenda kupata, hivyo hivi karibuni tutaendelea na utekelezaji wa mradi huu ili kuona kwamba maji yanapatikana.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji Igando - Kijombe ili kupunguza changamoto ya maji Jimbo la Wanging’ombe?

Supplementary Question 2

MHE. INNOCENT. S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza niishukuru Serikali kwa juhudi za kuendelea kuwapatia maji wananchi wa Jimbo la Kyerwa lakini tunao mradi wa Kyelwa, Nyaruzumbura, Nyakatuntu mpaka Kamuli, mradi huu tumeupitisha kwenye bajeti iliyopita lakini mpaka sasa mradi huu haujaanza, je, ni lini utaanza?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bilakwate, Mbunge wa Jimbo la Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi hii yote ambayo mtaji wake ni ukubwa bado tunaendelea kuona kwamba tunapata fedha na kwenda kuitekeleza. Hivyo, nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge Bilakwate tunakwenda kuutekeleza huu mradi na si kwa kuona kwamba tunatekeleza tu wajibu wetu, bali tunazingatia pia uhai kwa sababu maji ni uhai.

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji Igando - Kijombe ili kupunguza changamoto ya maji Jimbo la Wanging’ombe?

Supplementary Question 3

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naipongeza Wizara ya Maji kwa miradi inayotekelezwa ndani ya Jimbo la Mkenge Wilaya Misenyi, lakini miradi hiyo ya Igayaza, Byamte, Baishozi, Rutunga na Lwamachi Nakitobo imesimama kwa sababu ya kasi ndogo ya wakandarasi kwa kukosa fedha ambapo wameshaomba certificate Wizara ya Maji. Je, ni lini sasa wakandarasi hawa watalipwa ili miradi iweze kukamilika kwa wakati?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kyombo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tayari wiki iliyopita tumeanza kulipa wakandarasi, hivyo huenda na mkandarasi huyo akawemo ndani ya ile listi na tunaendelea kulipa. (Makofi)

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji Igando - Kijombe ili kupunguza changamoto ya maji Jimbo la Wanging’ombe?

Supplementary Question 4

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, asanye Mradi wa Matamba Kinyika ni mradi ambao ulikuwa unatekelezwa kwa bilioni nne lakini Mheshimiwa Waziri Aweso amepambana hadi umetekelezwa kwa bilioni mbili, lakini mradi huu una miaka minne na hadi sasa haujakamilika. Wananchi wa Kitongoji cha Itani, Mlondwe, Ngonde na Nungu bado wanahangaika na maji kupitia mradi huu. Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi huu ili wananchi wao wapate maji ya uhakika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nipokee shukrani, salamu za pongezi kwa niaba ya Waziri. Mradi huu kama alivyosema kwa jitihada za Mheshimiwa Waziri ameweza kuona kwamba ameupunguza na sasa hivi tutaendelea kuleta fedha ili kuona kwamba tunaenda kuukamilisha hivi punde, kama si ndani ya mwaka huu wa fedha kufika Juni, kabla ya mwaka 2022 kwisha tutahakikisha kwamba tunakuja kufanya kazi kwa sehemu kubwa.