Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini maji kutoka Ziwa Victoria yatafika katika Mji wa Tarime, Sirari, Nyamwaga na Nyamongo?

Supplementary Question 1

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nikiri kwamba Wizara ya Maji imetutendea haki Tarime angalau hali ya maji imeboreshwa. Nisipompongeza Mheshimiwa Waziri Aweso na Naibu wake itakuwa sijawatendea haki. Pamoja na kazi nzuri ambayo imefanyika naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza ni kwamba pale Sirari kuna mradi wa maji ambao tathmini ilifanyika ya kwanza ilikuwa shilingi 1,200,000,000, lakini tukarudia tathmini tukapata shilingi 534,000,000, sasa mradi unaendelea vizuri, imebaki shilingi 70,000,000 tu ili mradi ukamilike. Naomba nijue ni lini Serikali itapeleka fedha hizo pale mradi ukamilike Sirari ambapo ina wapigakura zaidi ya 17,000 ambao ndio ushindi wangu? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ningependa tu nijue kwamba ni lini sasa huu Mradi wa Ziwa Victoria utaanza kwa sababu hili ni swali muhimu sana kwa Mbunge wa Tarime Vijijini, Sirari, Nyamongo na Nyamwaga lini mwaka wa fedha huu, mwaka wa fedha ujao au upi, ni lini? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwita Mwikwabe Waitara, Mbunge wa Tarime Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nipende kupokea shukrani kwa namna ambavyo tunaendelea na kazi mbalimbali kwenye miradi mingi kote nchini lakini hususan kwenye Jimbo la Tarime Vijijini.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu ambao bado tu milioni 60 upo kwenye mchakato na mgao ujao kwa maana ya mwezi huu wa tano tutahakikisha tunawaletea hii milioni 60 ili mradi ukamilike, lengo ni kuona maji yanatoka bombani na tunawatua akinamama ndoo kichwani.

Mheshimiwa Naibu Spika, miji 28 tunatarajia kuanza kutekeleza hivi karibuni, tayari kile kipingamizi ambacho kilikaa kwa muda mrefu kimekwisha. Kipekee nipende kumpongeza na kumshukuru sana Mheshimiwa Rais mama Samia Suluhu Hassan kwa sababu ameingilia kati na sasa hivi tunakwenda vizuri, ni mfupa wa muda mrefu, lakini mama Samia ameweza kuutafuna, tunakwenda kuanza kazi katika miji 28.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini maji kutoka Ziwa Victoria yatafika katika Mji wa Tarime, Sirari, Nyamwaga na Nyamongo?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona. Wilaya ya Ngara ina vyanzo vikuu vya maji ambavyo ni Mto Ruvugu na Mto Kagera. Pamoja na uwepo wa vyanzo hivi tatizo la maji katika Wilaya ya Ngara limekuwa ni kubwa mno.

Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kujenga mradi mkubwa unaotosheleza wananchi wa Wilaya Ngara? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum, kutoa Mkoa wa Kagera kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Ngara ni moja ya wilaya ambayo tumeipa jicho la kipekee kabisa kuona kwamba tunaenda kutatua changamoto za maji. Niseme tayari tuna miradi ambayo ipo kwenye utekelezaji, lakini tuna miradi ambayo tutaendelea nayo hivyo tatizo la maji linakwenda kukoma.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini maji kutoka Ziwa Victoria yatafika katika Mji wa Tarime, Sirari, Nyamwaga na Nyamongo?

Supplementary Question 3

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Miradi ya Maji ya Wilaya ya Nkasi imekuwa ikusuasua sana pamoja na Mradi wa Namenyere ambao Waziri aliahidi ndani ya Bunge kwamba utakamilika mwezi Desemba mwaka jana, mpaka leo mwezi wa Nne mradi huo haujaweza kuwanufaisha watu wa Wilaya ya Nkasi. Je, ni lini Serikali itaondokana na fikra za kutumia mabwawa badala ya kutumia Ziwa Tanganyika ambapo ni kilomita 64 tu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Nkasi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kadiri tutakavyopata fedha tutakwenda kutumia Ziwa Tanganyika kukamilisha miradi ya maji.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini maji kutoka Ziwa Victoria yatafika katika Mji wa Tarime, Sirari, Nyamwaga na Nyamongo?

Supplementary Question 4

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Mkoa wa Katavi una miradi mingi midogomidogo ambayo imeletwa na Serikali na tunaipongeza, lakini mwarobaini wa Mkoa wa Katavi kuepukana na miradi hiyo midogomidogo ni kuleta Mradi wa Maji wa kutoka Ziwa Tanganyika kuleta makao makuu, je, ni lini mradi huu utaanza kufanyiwa kazi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kakoso, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Katavi ni moja ya eneo ambalo litakwenda kunufaika na maji kutoka Ziwa Tanganyika kama nilivyojibu kwa Mbunge wa Nkasi, tutakapopata fedha hii ni miradi yetu ya kimkakati tutakwenda kutekeleza.

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini maji kutoka Ziwa Victoria yatafika katika Mji wa Tarime, Sirari, Nyamwaga na Nyamongo?

Supplementary Question 5

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Ni lini bonde la Maji la Mitema ambalo lipo Jimbo la Newala Vijijini ambalo lina maji ya kutosha litafanyiwa kazi ipasavyo ili wananchi wa Newala, Tandahimba na Nanyamba waweze kupata maji ya uhakika kwa sasa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna, Mbunge wa Jimbo la Newala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mikoa ya kusini tunakwenda kuinufaisha na miradi yetu mikubwa ya Mto Ruvuma pamoja na maeneo yote ambayo yanatupatia maji ya kutosha. Hivyo bonde la maji la Mto Mitema nalo lipo kwenye mikakati yetu na kuona kwamba maeneo yote ya Newala tunakwenda kuondokana na maji ya kuokota na maji aina zote ambayo hayafai kwa matumizi ya wanadamu. (Makofi)

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini maji kutoka Ziwa Victoria yatafika katika Mji wa Tarime, Sirari, Nyamwaga na Nyamongo?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa
Naibu Spika, ahsante sana. Mji Mdogo wa Gairo ni mji ambao una matatizo ya maji, sasa naomba kujua Mradi wa Maji wa kutoka kwenye Milima ya Nongwe ni lini utakamilika ili wananchi wa Gairo waweze kupata maji ya kutosha?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Morogoro, Mwenyekiti wetu wa Kamati ya Maji, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi hii anayoiongolea uendelevu wake unatokana na mapato ya fedha, kwa hiyo kadri tutakavyoendelea kupata fedha, namna ambavyo tumekuwa tukipeleka fedha nyingi sana kwenye maeneo yote, tutapeleka fedha kwani na Gairo pia tunatamani waondokane na tatizo la maji.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini maji kutoka Ziwa Victoria yatafika katika Mji wa Tarime, Sirari, Nyamwaga na Nyamongo?

Supplementary Question 7

MHE. SHABAN O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Takribani miaka sita sasa imepita katika Kata ya Kwai iliahidiwa na Serikali mradi wa maji lakini mpaka sasa mradi ule hakuna chochote kilichofanyika. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji katika Kata ya Kwai ili wananchi waondokane na adha hii wanayoendelea kuipata sasa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kata zake nyingi katika jimbo tumeshazishughulikia, hivyo hata kata hii ipo katika mkakati wa kuona kwamba na wao wanaenda kupata maji safi na salama ya kutosha. Tukishindwa kukamilisha ndani ya mwaka huu wa fedha basi mwaka ujao wa fedha tutahakikisha hii kata nayo inakwenda kunufaika na kumtua mama ndoo kichwani.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: - Je, ni lini maji kutoka Ziwa Victoria yatafika katika Mji wa Tarime, Sirari, Nyamwaga na Nyamongo?

Supplementary Question 8

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Swali langu, ni lini sasa kituo cha afya kinachoitwa Malawi kilichopo Yombo Vituka kitapata maji? Tumepata vifaa vizuri sana vya ndani ya hospitali lakini maji tunayotumia ni ya visima, leo na tuko mjini.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kilave, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kutoa huduma ya maji katika maeneo kama ya hospitali, shule ni moja ya vipaumbele vyetu.

Kwa hiyo maeneo haya ambayo bado yanatumia maji ya visima tunatoa kipaumbele na tutahakikisha kwenye kituo cha afya tutapeleka maji safi na salama bombani kwa lengo la kuona kwamba wanaendelea kuishi kwenye karne ya mama Samia kwa sababu Serikali ya Mama Samia imeweza kutoa fedha nyingi kwenye miradi ya maji.