Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 34 2022-04-11

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: -

Je, ni lini maji kutoka Ziwa Victoria yatafika katika Mji wa Tarime, Sirari, Nyamwaga na Nyamongo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwita Mwikwabe Waitara, Mbunge wa Tarime Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu la Serikali ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama na yenye kutosheleza. Katika mipango ya muda mfupi ya kupunguza kero ya uhaba wa maji katika Wilaya ya Tarime, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imekamilisha Miradi ya Maji ya Sirari na Nyamwaga na inaendelea kutekeleza Miradi ya Nyangoto (Nyamongo), Sabasaba na Gimenya (Mjini Tarime). Miradi hiyo inatarajia kukamilika mwezi Juni, 2022 ambapo hali ya huduma ya maji katika Mji wa Tarime itaimarika kutoka asilimia 45 hadi asilimia 56 na maeneo mengine ya Wilaya ya Tarime kutoka asilimia 70 hadi asilimia 75.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mpango wa muda mrefu, Wilaya ya Tarime itanufaika na Mradi wa Kuboresha Huduma ya Maji katika Miji 28 ambapo chanzo cha maji cha Ziwa Victoria kitatumika. Kupitia Mradi huo Miji ya Tarime, Sirari, Nyamwaga na Nyamongo na maeneo mengine ya Wilaya ya Tarime yatanufaika na lengo la asilimia 85 vijijini na 95 mijini litafanikiwa ifikapo mwaka 2025.