Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA K.n.y. MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, ni watumishi wangapi wamesimamishwa kazi tangu mwaka 2015 hadi 2022 ambao mashauri yao hayajaisha?

Supplementary Question 1

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niulize swali moja dogo la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwepo na changamoto kubwa kwa watumishi wa umma hasa hawa ambao mashauri yao yanaendelea kusikilizwa kwamba yanachukua muda mrefu sana na hii inawanyima haki kama watumishi wa umma. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha haya mashauri yanakamilika kwa wakati? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Godwin Kunambi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyotoa maelezo kwenye majibu yangu ya msingi, mashauri ambayo yapo, ya watumishi wanaotakiwa kuchukuliwa hatua za kinidhamu ni watumishi 1,477; mashauri yaliyokuwa kwenye Tume ya Utumishi wa Umma ni mashauri 598; na kati ya rufaa hizi ambazo zimetajwa kule Tume ya Utumishi wa Umma, rufaa 411 zina vielelezo vilivyokamilika; na rufaa 187 hazina vielelezo, kwa hiyo, zimerudishwa kwa waajiri na mamlaka za nidhamu ili ziweze kufanyiwa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, rai yangu kama nilivyoitoa awali, ni kwamba hawa ambao wanapeleka mashauri Tume ya Utumishi wa Umma hayana vielelezo, yaweze kuwa yamewasilishwa na vielelezo kamili ili haki ya watumishi ambao Mheshimiwa Kunambi ameizungumzia hapa, iweze kupatikana kwa haraka zaidi. (Makofi)

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA K.n.y. MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, ni watumishi wangapi wamesimamishwa kazi tangu mwaka 2015 hadi 2022 ambao mashauri yao hayajaisha?

Supplementary Question 2

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumwuliza Waziri swali la nyongeza kwamba kulikuwa na watumishi wa Darasa la Saba ambao wamesimamishwa na walikuwa wamefanya kazi kwa muda mrefu na baadaye hawakupewa kiinua mgongo wala chcohote: Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu watumishi hawa ambao kwa kweli wametumikia pia Taifa kwa kipindi kirefu kwa ujuzi huo wa Darasa la Saba? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI
WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Noah, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, watumishi wa darasa la saba walioajiriwa baada ya Mei, 2004 wale Serikali ilikwishatoa tamko na ilimradi wawe walikuwa hawakughushi nyaraka zao walipewa muda mpaka ifikapo Desemba, 2020 wawe wamejiendeleza na kuweza kuendelea na ajira zao na wale ambao hawakujiendeleza, tayari mamlaka ilishatoa tamko kwamba wale washughulikiwe walipwe michango yao ya hifadhi ya jamii.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hadi kufikia Desemba, 2020 jumla ya watumishi 1,191 walikuwa hawakujiendeleza na hivyo wanastahili kulipwa michango yao ya hifadhi ya jamii.