Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 4 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 33 2022-04-11

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA K.n.y. MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: -

Je, ni watumishi wangapi wamesimamishwa kazi tangu mwaka 2015 hadi 2022 ambao mashauri yao hayajaisha?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Godwin Emmanuel Kunambi, Mbunge wa Mlimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, usimamizi wa nidhamu katika Utumishi wa Umma ni suala muhimu ambalo limeainishwa katika Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura 298; Kanuni za Utumishi wa Umma za Mwaka 2003; Taratibu za Uendeshaji katika Utumishi wa Umma za Mwaka 2003; Taratibu Bora za Nidhamu katika Utumishi wa Umma za Mwaka 2007 na Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma za Mwaka 2009.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha mwaka 2015 hadi mwaka 2022, idadi ya watumishi waliosimamishwa kazi katika Taasisi mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na Mamlaka za Serikali za Mitaa, pamoja na Serikali Kuu ambao mashauri yao hayajahitimishwa ni watumishi 836. Watumishi hawa ni miongoni mwa watumishi 1,477 waliokuwa wamesimamishwa kazi kwa kukiuka sheria, kanuni, taratibu na miongozo inayosimamia nidhamu katika Utumishi wa Umma. Mashauri haya yapo katika hatua mbalimbali za mamlaka za nidhamu ambazo ni waajiri mbalimbali na mamlaka za rufaa ambazo ni Tume ya Utumishi wa Umma, Tume ya Walimu na Ofisi ya Rais.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kuwakumbusha Waajiri/Mamlaka za Nidhamu kuongeza kasi ya kuhitimisha mashauri ya nidhamu yaliyopo kwa kuzingatia taratibu za uendeshaji wa mashauri ya kinidhamu.