Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohammed Said Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wa Kituo cha Polisi cha Konde katika Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED SAID ISSA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwanza, niishukuru Wizara kwa kuweza kutenga fedha kwa ajili ya matengenezo ya Kituo cha Konde, lakini swali langu la nyongeza ni kwamba katika Kituo cha Polisi cha Konde pia kuna nyumba za askari ambazo wanatumikia katika kituo kile. Je, Serikali ina mpango gani wa kuweza kuzikarabati?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, pia katika maeneo ya Konde mbele kuna Kituo cha Polisi kinaitwa Matangatuani ambacho ni kituo muhimu sana kinatumika kwa ajili ya ulinzi wa mali, lakini pia na uhalifu kwa sababu Jimbo la Konde ni la mpakani, Je Serikali ina mpango gani wa kuweza kukikarabati Kituo hicho cha Matangatuani?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mohamed Saidi Issa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu kukarabati nyumba za askari zilizo kwenye kituo hicho, hili ni jambo muafaka kabisa tunapokuwa tunafanya tathmini hizi gharama zinazohitajika kwa ajili ya ukarabati wa kituo tutazingatia nyumba hizo ili ziweze kuingizwa katika mpango wa ukarabati.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili la kuboresha kituo cha polisi kilicho mpakani, Matangatuani, tutakifanyika tathmini kituo hicho ili kuona kiwango cha fedha zinazohitajika kwa ajili ya ukarabati wake, tuweze kukiingiza katika mpango wetu wa ukarabati. Nashukuru. (Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wa Kituo cha Polisi cha Konde katika Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale haina Kituo cha Polisi na kwa kuliona tatizo hilo nimetoa fedha shilingi 10,000,000 kutoka kwenye Mfuko wa Jimbo kwa ajili ya kuanza ujenzi. Je, Serikali inatusaidiaje ili kuimarisha kituo cha Polisi cha Wilaya ya Liwale? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Mbunge Kuchauka kwa kuchangia shilingi 10,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi Liwale, naomba nitoe ahadi kama nilivyosema katika swali lililopita kwamba maeneo yote ya Wilaya ambayo hayana Vituo vya Polisi ni mpango wa Serikali kuona kwamba Wilaya hizo zinapata Vituo vya Polisi, hivyo tutafanya tathmini kuona kiwango cha fedha kinachohitajika ili kushirikiana nae tuweze kukamilisha Kituo cha Polisi Liwale. (Makofi)

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wa Kituo cha Polisi cha Konde katika Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 3

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Singida Mjini ni Mji ambao unakuwa kwa kasi sana na maeneo mengi hayana vituo vya Polisi hali inayopelekea askari wetu kusafiri kwa umbali mrefu. Je, Serikali haioni haja sasa umefika wakati wa kuwaongezea walau fedha ya mafuta ili waweze kufanya kazi yao vizuri ya usalama wa raia?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mussa Sima, Mbunge wa Singida Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba Makao Makuu ya Mikoa yetu mingi kwa kweli yanapanuka sana na kuhitaji huduma za kipolisi kwa maana ya kuwa na magari, kuelekea kwenye maeneo hayo kuwahudumia wananchi. Niseme kama itakavyokuja kusomwa bajeti yetu hapa mwaka huu Rais wa Awamu ya Sita, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, ameongeza fedha kwenye majeshi yetu ikiwemo Jeshi la Polisi ili kuimarisha shughuli za kiulinzi ikiwemo doria na mambo kama hayo. Kwa hiyo Wilaya ya Singida na Manispaa ya Singida ni moja ya Wilaya zitakazonufaika na ongezeko hilo la Bajeti. (Makofi)

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wa Kituo cha Polisi cha Konde katika Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 4

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nina swali moja; kwa vile Vituo vya Polisi vya Kibara, Bulamba na Kisorya vinatumia nyumba za wenyeji kufanyia kazi zake. Je, ni lini Serikali itajenga vituo hivyo? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kajege, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Kajege kwa juhudi zake za kuimarisha huduma za ulinzi wa wananchi ikiwemo kuhamasisha wananchi kushiriki kujenga vitu vya Polisi vya Bulamba na Kisorya. Napenda kumuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutafanya tathmini ya kiwango cha fedha zinazohitajika kukamilisha vituo hivyo ili viweze kuingizwa katika mpango na bajeti itakayosomwa siku zijazo. Nashukuru.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wa Kituo cha Polisi cha Konde katika Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 5

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati mkubwa katika Kituo cha Central kilichopo Jimbo la Tabora Mjini? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Mwaifunga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Vituo Vikuu vya Polisi vya Mikoa kama anavyosema Central Tabora vinahitaji kufanyiwa tathmini kwa ajili ya kuona mahitaji ya fedha yanayohitaji kwa ajili ya kuwezesha ukarabati huo kufanyika. Naomba nimuahidi Mheshimiwa Mwaifunga na bahati nzuri Tabora ni eneo nililoanzia kazi, tutashirikiana na Mheshimiwa Mbunge na Mbunge wa Jimbo ili kufanya tathmini ya kiwango cha fedha zinazohitajika ili ukarabati huo uweze kufanywa. (Makofi)

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wa Kituo cha Polisi cha Konde katika Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 6

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Kibiti inafahamika maarufu sana kwa jina la Kanda Maalum, sasa ni upi mpango wa Serikali kujenga Kituo cha Polisi ambacho kina hadhi ya Kanda Maalum katika Wilaya ya Kibiti? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Twaha, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua ulianzishwa Mkoa wa kipolisi Kanda Maalum ya Kibiti, ukaanza kwa utaratibu wa dharura kwa kutumia ofisi ya OCD zilizokuwepo miongoni mwa Mikoa mipya ya kipolisi ambayo itajengewa majengo yake ni pamoja na Mkoa huu wa Kanda Maalum ya Kibiti. Kwa hivyo Mheshimwia Mbunge asubiri kadri tutakapokuwa tunapata fedha, Kibiti itapewa msisitizo maalum. (Makofi)