Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 3 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 28 2022-04-08

Name

Mohammed Said Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati wa Kituo cha Polisi cha Konde katika Wilaya ya Micheweni?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Saidi Issa, Mbunge wa Konde, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uchakavu wa Kituo cha Polisi cha Konde ambacho jengo lake lilijengwa wakati wa ukoloni. Tathmini kwa ajili ya ukarabati wa kituo hicho imefanyika na kubaini kwamba kiasi cha fedha Sh.42,000,000/= kinahitajika ili kugharamia ubadilishaji paa, kubadilisha mfumo wa umeme, maji safi na maji taka, kuziba nyufa, kubadilisha dari na kupaka rangi. Ukarabati huo utafanyika kulingana na upatikanaji wa fedha. Aidha, Serikali inawahamasisha wadau walio tayari kushirikiana na Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Wilaya katika kuboresha vituo vya Polisi vilivyo kwenye maeneo yao.