Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapitia gharama za leseni kwa Wabunifu wa Apps za huduma za kifedha na kuwawezesha kutumia mifumo iliyopo?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Spika,
nianze kwa ushauri mdogo kwamba Serikali iende ikaziangalie hizi gharama, bado ni kubwa sana na zinadumaza ubunifu. Maswali mawili yangu ya nyongeza; vijana wengi wamejiajiri kupitia ubunifu na wengi wanafanyakazi na taasisi za nje, changamoto imekuwa ni malipo.

Je, ni lini sasa Serikali itaruhusu mfumo wa pay poll ili vijana hawa ambao wamejiajiri na kufanya kazi za consultancy huko nje ya nchi waweze kupata malipo yao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; tuna vijana wengi wabunifu ambao wanaandaa mifumo ya software. Software ambazo tunazinunua online hazitozwi VAT, lakini zile ambazo zinatengenezwa nchini, zinatozwa VAT. Ni lini sasa Serikali itafanya mapitio ili kuhakikisha kwamba wabunifu wa ndani ya nchi wanapata nafuu katika mifumo ambayo wanaitengeneza hapa nchini? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ndugulile kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote naomba kumpongeza sana Mheshimiwa Ndugulile kwa kiasi ambacho anapigania wananchi wa Jimbo la Kigamboni na Watanzania kwa jumla. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mfumo wa Paypal bado haujazuiliwa na unaendelea kutumika nchini. Mwaka 2016 wawakilishi wa Paypal walifika Benki Kuu ya Tanzania ili kupata taratibu zinazotakiwa katika kutekeleza huduma hiyo. Hata hivyo, Serikali ipo tayari kupokea maombi ya leseni kwa sababu hawawezi kuendesha huduma hiyo bila kuwa na leseni. Serikali iko tayari kupokea leseni hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, ni kweli kabisa. Naomba nikiri kwamba ni kweli huduma hii ya software au huduma za mtandao hulipiwa VAT ni suala la kweli kabisa kwamba lazima ilipiwe VAT na ni tofauti, yaani VAT ambayo inalipiwa kwa software ambazo zinatengenezwa nchini, zinakuwa na ongezeko hilo la thamani tofauti na ambazo wananunua ndani ya mtandao online.

Mheshimiwa Spika, suala hili tayari utafiti umeshafanyika kwa kina na mapendekezo yake tayari. Nalihakikishia Bunge lako Tukufu kwamba mapendekezo hayo yatawasilishwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/ 2023 mwaka huu. Ahsante. (Makofi)

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapitia gharama za leseni kwa Wabunifu wa Apps za huduma za kifedha na kuwawezesha kutumia mifumo iliyopo?

Supplementary Question 2

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Makampuni mbalimbali ya simu yanatoa huduma za mikopo kupitia mitandao na riba zake ziko juu sana: -

Je, Benki Kuu inafanya nini kuhakikisha inasimamia huduma hizi?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Benki Kuu ya Tanzania inapitia maombi yote ambayo yanaletwa na makampuni mbalimbali. Itakapojiridhisha, basi itatoa leseni kwa kampuni yoyote ikizingatia masharti kwamba lazima waambatane au washirikiane na kampuni au taasisi ambayo ipo ndani ya nchi yetu. (Makofi)