Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 3 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 25 2022-04-08

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapitia gharama za leseni kwa Wabunifu wa Apps za huduma za kifedha na kuwawezesha kutumia mifumo iliyopo?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Faustine Engelbert Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Mifumo ya Malipo ya mwaka 2015 inazitaka kampuni zinazotaka kuendesha huduma za malipo kuwa na leseni ya kutoa huduma inayosimamiwa na sheria hiyo. Leseni hii hutolewa na Benki Kuu ya Tanzania mara baada ya kampuni kukamilisha taratibu zote za kupata leseni. Kampuni ikikamilisha taratibu zote, hutakiwa kufanya malipo ya leseni ambayo ni shilingi milioni 12 na hufanyika mara moja kila baada ya miaka mitano. Aidha, Sheria ya Mifumo ya Malipo inakataa kutoa huduma za malipo bila leseni na adhabu zake zimeainishwa kwenye vifungu vya sheria husika.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia mwenendo wa maombi ya leseni kutoka kampuni mbalimbali za huduma za malipo na kiwango cha uwekezaji wa kampuni hizo, ni maoni ya Serikali kuwa gharama za leseni kwa wabunifu wa App za huduma za kifedha zinaendana na mahitaji ya soko. Naomba kuwasilisha. (Makofi)