Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kubebea Wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mkalama?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante, na ninamshukuru Mhehsimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri naomba niulize maswali madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; ni lini Serikali itapeleka magari ya wagonjwa kwa Hospitali ya Ilongelo na Hospitali ya Wilaya ya Manyoni iliyopo Singida?

Mheshimiwa Spika, swali la pili vituo vya afya vya Ngome na Ipogolo vimekuwa vikitumia magari ya abiria katika kusafirisha wajawazito kwenda kujifungu. Ni lini sasa Serikali itaona umuhimu pia wa kutupatia magari katika hospitali yetu ya Wilaya ya Iringa Manispaa na katika vituo hivyo vya Afya vya Iringa Mjini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ritta Kabati Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimetangulia kujibu kwenye jibu langu la msingi, kwamba Serikali itanunua magari ya wagonjwa 195 kwa ajili ya Halmashauri zetu zote 184 nchini kote. Kwa hivyo Kituo cha Afya na Hospitali ya Ilongelo na Manyoni zitanufaika kwa magari hayo lakini bado tutaendelea kutenga fedha kwa awamu ili vituo vingine vyote vipate magari ya wagonjwa, kwa maana ya kuboresha huduma za rufaa.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na Kituo cha Afya cha Ngumi, Ipogolo na Hospitali ya Manispaa ya Iringa ni kweli ina changamoto ya gari la wagonjwa; na Manispaa ya Iringa nayo itanufaika na magari haya. Kwa hiyo changamoto hiyo kwa sehemu itakuwa imetatuliwa, lakini tutaendelea kutafuta magari zaidi.

Mheshimiwa Spika, tarehe 06 juzi Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan amezindua mpango mkakati wa M-mama ambao utawezesha rufaa za dharura katika mikoa 12 kwa kushirikisha wadau, wakiwemo Vodacom. Kwa hiyo pamoja na jitihada za Serikali lakini bado jitihada za private sector kama Vodacom tutakwenda kuondoa kabisa changamoto ya rufaa kwa wagonjwa wetu, ahsante sana.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kubebea Wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mkalama?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, asante sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza, nikiwa na hakika kabisa kwenye magari na Wilaya ya Hai itapata.

Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza ni lini Serikali sasa itatuletea vifaa tiba kwenye kituo chetu cha afya cha Longoi ambacho kimekamilika, ili kiweze kuanza kazi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe Mbunge wa Hai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali yetu imeendelea kutenga fedha za ununuzi wa vifaa tiba kwa awamu. Kwa sasa tayari imeshatenga kwa ajili ya Hospitali zile 67 za awamu ya kwanza lakini tutakwenda Hospitali zile 28 za awamu ya pili na vituo vya afya vitatengewa fedha baada ya kukamilika kwa hizi 67 na 28 kikiwemo Kituo hiki cha Afya katika Halmashauri ya Hai. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hicho ni kipaumbele cha Serikali na kadri ya upatikanaji wa fedha tutapeleka fedha na vifaa tiba katika Kituo cha Afya cha Hai.