Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 22 2022-04-08

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kubebea Wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mkalama?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aysharose Ndogholi Mattembe Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/ 2022 Serikali kupitia Mpango wa Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO-19 itanunua magari 195 ya kubebea wagonjwa ambayo yatagawiwa kwa Halmashauri zote 184. Kupitia utaratibu huu kila Halmashauri itapatiwa gari moja la kubebea wagonjwa, ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa magari ya kubebea Wagonjwa ili kuboresha na kuimarisha hali ya utoaji huduma za afya nchini kote.