Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Paulina Daniel Nahato

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa vibali kwa Vyuo Vikuu vyenye upungufu wa Wahadhiri ili viweze kuajiri Wahadhiri wapya?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, namshukuru Waziri kwa majibu mazuri, lakini naomba kumuuliza maswali mawili.

Tunafahamu Serikali inaenda kutekeleza Mradi wa High Education for Economic Transformation (HEET); sasa namuuliza swali; je, mradi huo unatarajia kusomesha wahadhiri wangapi?

Je, Serikali inatuhakikisha kuwa Mradi huu wa HEET utapunguza uhaba wa Wahadhiri katika vyuo vikuu kwa kiasi gani? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba sasa kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Nahato kwa pamoja kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali yetu ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wetu, Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan, tumepata mkopo wa jumla ya dola za Kimarekani milioni 425, sawa na shilingi bilioni 972.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mradi huu, pamoja na mambo mengine utakwenda kuimarisha miundombinu kwenye vyuo vyetu vya Umma karibu 14, vilevile utashughulikia masuala ya Wahadhiri pamoja na watafiti katika nchi yetu. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu, katika mradi huu tunatarajia kufanya maendelezo ya Wahadhiri wetu katika Vyuo Vikuu wapatao 831, ambapo katika kada ile ya PhD., ambayo tunaita Uzamivu, ni wahadhiri 444 na wale wa Masters yaani Uzamili ni 387.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi, jambo hili tutakwenda kulifanya na kuhakikisha tunataondoa changamoto hii ya wahadhiri katika vyuo vyetu. Nakushukuru. (Makofi)

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa vibali kwa Vyuo Vikuu vyenye upungufu wa Wahadhiri ili viweze kuajiri Wahadhiri wapya?

Supplementary Question 2

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nimesikia majibu ya Serikali ni mazuri na yanaleta moyo katika kupunguza changamoto ya upungufu wa Wahadhiri na hasa Wahadhiri Wabobezi katika Vyuo Vikuu vyetu. Pamekuwa na tafiti chini ya Chama cha Wafanyakazi wa Vyuo Vikuu (THTU) kwamba kuna upungufu mkubwa sana; utafiti wa 2017, lakini sababu kubwa waliyotoa ni Serikali kutumia sana wataalamu wao katika kujaza nafasi mbalimbali Serikalini: -

Je, Serikali haioni sasa ni wakati mzuri wa kushauri mamlaka za uteuzi kuacha kutumia wataalam hawa, hasa Wahadhiri Wabobezi katika nafasi mbalimbali Serikalini?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mtemvu, Mbunge wa Kibamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa vile Mbunge ametoa wazo na Mamlaka za Uteuzi zipo, namwomba Mheshimiwa Mbunge tuichukue hoja yake hii ili tuweze kuifikisha kwenye vyombo hivi vya uteuzi ili waweze kufanya evaluation au tathmini toshelezi kabisa iwapo kama wanaona inafaa kufanya hivyo, basi liweze kufanyiwa kazi. Nakushukuru sana.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa vibali kwa Vyuo Vikuu vyenye upungufu wa Wahadhiri ili viweze kuajiri Wahadhiri wapya?

Supplementary Question 3

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, ahsante sana. Kumekuwa na uhaba mkubwa sana wa Maprofesa katika Vyuo Vikuu vya Dar es Salaam, Sokoine, Mandela, Ardhi na Chuo cha Muhimbili. Baada ya kustaafu wakiwa na miaka 65 wanaambiwa waende nyumbani na biashara imeishia hapo, lakini kuna uhaba mkubwa.

Kipi bora, je, tuongeze miaka yao ifike angalau 70 waendelee kuhudumia nchi yetu? Kwa sababu kuna ombwe kubwa sana la ngazi hizi kwenye Vyuo Vikuu. Naomba Serikali ifikirie hawa watu waendelee mpaka miaka fulani hivi ili vijana wetu wapate elimu ya uhakika. Ahsante sana.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Profesa Ndakidemi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli anayozungumza Mbunge kwamba tumekuwa na changamoto sana ya Wahadhiri katika kada hii ya Maprofesa kutokana na wao kustaafu. Naomba nimweleze tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kustaafu kwa upande wa Utumishi wa Umma ilikuwa ni miaka 60 kwenye maeneo mengine yote, lakini kwa upande wa wenzetu hawa Maprofesa au Wahadhiri wa Vyuo Vikuu ilipandishwa kutoka miaka 60 kwenda miaka 65. Sasa hivi Mheshimiwa Profesa Ndakidemi anasema kwamba angalau tungeongeza ifike miaka 70.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba tulibebe wazo hili, ingawa vilevile nimeeleza kwenye majibu yangu ya msingi kwamba katika mradi wetu wa HEET, unakwenda kufundisha katika level ile ya Ph.D ambapo tunaamini wengi sasa wataenda kuwa Maprofesa, ambao tutahakikisha katika eneo hili tunaenda kufanya coverage kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuchukue wazo lake Mheshimiwa Prof. Ndakidemi twende tukalifanyie kazi ili tuweze kuona mtu akifikisha miaka 70 atakuwa na uwezo wa kusimama darasani akafundisha au akasimamia watu kwenye kazi zao? Nakushukuru sana. (Makofi)