Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 2 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 20 2022-04-06

Name

Dr. Paulina Daniel Nahato

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PAULINA D. NAHATO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa vibali kwa Vyuo Vikuu vyenye upungufu wa Wahadhiri ili viweze kuajiri Wahadhiri wapya?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Paulina Daniel Nahato Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua changamoto ya upungufu wa Wahadhiri katika Vyuo Vikuu vya Umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekua ikitoa vibali vya ajira kila mwaka ambapo katika mwaka wa fedha 2018/ 2019 hadi 2020/2021, Serikali ilitoa vibali vya nafasi za ajira mpya za Wakufunzi na Wahadhiri Wasaidizi 333 katika Vyuo Vikuu vya Umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa Wahadhiri Vyuoni, Wizara yangu inaendelea na jitihada za kuomba vibali vya ajira za Wahadhiri kutoka Wizara yenye dhamana na Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Sambamba na hilo, pia upo utaratibu wa kuwahamisha watumishi wenye sifa kutoka Taasisi mbalimbali za Serikali kwenda Vyuo Vikuu na kuwajengea uwezo ikiwa ni pamoja na kuwasomesha kozi za muda mfupi na mrefu. Nakushukuru sana.