Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: - Je, ni Sheria gani inasimamia orodha ya wanaostahili kutumia ving’ora na vimulimuli kwa misafara ya Viongozi na Wananchi wa kawaida?

Supplementary Question 1

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Niishukuru Serikali kwa majibu mazuri na kwa operesheni inayoendelea maana Dar es Salaam ilikuwa kila ukikaa unasikia koro koro nyuma ya gari yako, kitu ambacho ni kinyume cha sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia Kifungu cha 54 cha Sheria, Sura ya 168 ya Usalama Barabarani; je, Waziri ameshatoa vibali vingapi mpaka sasa vya utumiaji wa ving’ora ukiondoa magari yaliyoorodheshwa?

Swali la pili; je, Serikali ina mpango gani wa kufanya marekebisho ya sheria hii ambayo ni ya muda mrefu ili kuweza kutoa adhabu stahiki kwa watu wanaovunja sheria hii, vilevile kuweza kuona namna ya kuongeza viongozi wenye kustahili heshima hii na kuweza kuwaondolea taharuki wananchi. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jerry Silaa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka sasa tokea nimepewa dhamana hii sijawahi kutoa kibali hata kimoja.

Pili, kuhusu mabadiliko ya sheria tunao mchakato ambao unaendelea wa mabadiliko ya sheria ya usalama barabarani, kwa hiyo kwa kuwa mchakato huu hatma yake ni hapa Bungeni, basi Mheshimiwa Mbunge naomba hoja zake aziandae vizuri ili kuweza kuhakikisha mchakato huu utakapofika Bungeni aweze kusaidia kutoa hoja za kuongeza yale ambayo anahisi yanafaa katika marekebisho hayo ya sheria itakapokuja. (Makofi)