Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 18 2022-04-06

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA aliuliza: -

Je, ni Sheria gani inasimamia orodha ya wanaostahili kutumia ving’ora na vimulimuli kwa misafara ya Viongozi na Wananchi wa kawaida?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jerry William Silaa Mbunge wa Ukonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Usalama Barabarani Sura ya 168 ya mwaka 1973 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002, ndiyo sheria inayosimamia matumizi ya ving’ora na vimulimuli barabarani. Kifungu 39(b) kifungu kidogo cha (1) na (2) cha sheria, kinaelekeza matumizi ya ving’ora na vimulimuli barabarani ambayo ni kutoa ishara kwa watumiaji wengine wa barabara kuchukua tahadhari kuwa kuna dharura. Kifungu cha 54 kifungu kidogo cha (1) hadi cha (5) kinaeleza utaratibu na mazingira ya matumizi ya ving’ora na vimulimuli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, magari yanayostahii kutumia ving’ora na vimulimuli kwa mujibu wa sheria ni magari ya polisi, zimamoto, magari ya wagonjwa (ambulance), magari ya vikosi vya ulinzi na usalama pamoja na magari yaliyopata kibali maalumu kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na kutangazwa katika Gazeti la Serikali.