Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza: - Je, Serikali ina kauli gani juu ya ushuru mkubwa wa bidhaa za ngozi unaotozwa bandarini na vikwazo vya kusafirisha bidhaa hiyo nje ya nchi?

Supplementary Question 1

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa majibu ya Waziri yanakiri kwamba ushuru mkubwa ulilenga kulinda viwanda vya ndani na ni asilimia 80 ya thamani ya mzigo ukiwa bandarini, sasa kuna ushahidi ulio dhahiri kwamba viwanda vya ndani vilivyokuwa vikilindwa vingi vimekufa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna kiwanda cha Himo ambacho na chenyewe kiko hai, lakini ngozi inayohitajika ni ya kilogram 12 ambayo inapatikana Bukoba. Sasa swali langu kwa Serikali, wafanyabiashara wa ngozi wamekwama ushuru mkubwa, viwanda vya ndani vimekufa, Serikali haipati mapato ya kutosha. Sasa, je, kwa kuzingatia kwamba hata Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki linapokuja suala la masilahi ya ndani na yenyewe wala haitekelezi makubaliano yenu, kwa nini Serikali isifanye tathmini upya, kuangalia uamuzi wake ili kulinda wafanyabiashara wa ndani wa Ngozi na kulinda nchi? Hilo swali langu la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, tunaingia mwaka mpya wa fedha, tunaamini Wizara ya Mifugo chini ya Mawaziri akiwemo kijana makini, hivi bado hawajafikiria mwaka huu wa kikodi kuangalia hili eneo muhimu? Kwa sababu ni dhahiri shahiri kuna ngozi zinaoza huko mtaani kwa maelfu, hawajaangalia hili eneo ili wasaidie nchi? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Halima James Mdee, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza ni juu ya tathmini Serikali kutazama kulingana na hali halisi ya biashara ya Ngozi. Nimelipokea jambo lake hili la kusema tufanye tathmini ni jambo jema.

Vilevile nimshukuru amekiri na ndio ukweli wenyewe kwamba tumeweka viwango hivi vya kikodi ndani ya Jumuiya yetu ya Afrika Mashariki kwa lengo la kulinda viwanda vyetu vya ndani. Hii 80 percent tuliyoiweka imewekwa makusudi kwa ajili ya ku-discarage kutoa ngozi ikiwa ghafi kwenda nje ya mipaka ya Taifa letu ili kulinda ajira na kupata kipato zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, niseme ukweli bado ngozi nyingi inakwenda nje ikiwa ghafi, pamoja na ushuru huo mkubwa inakwenda Nigeria, Ghana ambako huko wanaitumia kama chakula, kwa hiyo hili lifahamike. Hii ngozi tunayosema kwamba iko vijijini inaharibika, inawezekana lakini kwa uhitaji wa ngozi wa sasa jambo la ngozi kuharibika ni kiasi kidogo sana, yawezekana wahitaji wanaohitaji hizi ngozi hawajaweza kuvifikia vile vijiji ambavyo vina hiyo ngozi inayoharibika. Hata hivyo, niseme tu kwamba tutaimarisha sasa mfumo wetu ili hata ile iliyoko kule vijijini iweze kupatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, amezungumza juu ya maboresho ya kikodi. Hili jambo pia vilevile nimelichukua, kwa ajili ya kuweza kuangalia maslahi mapana ya sekta hii ya ngozi.