Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 2 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 15 2022-04-06

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza: -

Je, Serikali ina kauli gani juu ya ushuru mkubwa wa bidhaa za ngozi unaotozwa bandarini na vikwazo vya kusafirisha bidhaa hiyo nje ya nchi?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima James Mdee, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwango vya ushuru wa kusafirisha ngozi ghafi na ngozi iliyosindikwa kiwango cha kati kwa maana ya Wet blue nje ya nchi ni makubaliano ya Nchi Wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki waliokubaliana kuainisha viwango vya ushuru kwa lengo la kuhakikisha viwanda vya ndani vinapata malighafi ya kutosha na kuzalisha bidhaa za ngozi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushuru wa kusafirisha ngozi ghafi nje ya nchi kwa maana export levy ni asilimia 80 ya mzigo ukiwa bandarini kwa maana FOB au Dola za kimarekani 0.52 kwa kilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, ngozi zilizosindikwa kwa kiwango cha kati kwa maana ya Wet blue zinatozwa ushuru wa asilimia 10 ya FOB ili kutoa motisha kwa wasindikaji. Ngozi zilizosindikwa hadi kufikia hatua ya mwisho kwa maana ya finished leather hazitozwi ushuru wowote ule, ni 0%. Jitihada hizo zimesaidia kuvutia uwekezaji katika viwanda vya kusindika ngozi na kuzalisha bidhaa za ngozi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna vikwazo vyovyote katika kusafirisha zao la ngozi, kwa kuwa takwimu zinaonyesha kiwango cha usafirishaji wa ngozi ghafi kimeendelea kupanda kutoka kilo 513,201 mwaka 2015/2016 hadi kufikia kilo 7,370,533 mwaka 2020/2021.