Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Afya wa Kada mbalimbali katika Wilaya ya Kakonko?

Supplementary Question 1

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Pamoja na majibu ambayo yametolewa na Serikali na mpango mzuri wa Serikali katika kupeleka watumishi katika maeneo mbalimbali hasa Wilaya ya Kakonko, bado watumishi hawa wamekuwa wakihama kutokana na upungufu wa miundombinu hasa nyumba za watumishi katika maeneo hayo.

(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba watumishi hawa wa kada ya afya wanabaki katika maeneo hayo hasa kwa kujenga nyumba za watumishi hao?
(Makofi)

(b) Kutokana na changamoto hiyo: Je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kufuatana nami kwenda Wilaya ya Kakonko ili hiki ambacho nakieleza kama changamoto aweze kuona na hatimaye aweze kutafuta njia sahihi za kuweza kumaliza changamoto hiyo? Nashukuru. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Jimbo la Buyungu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza Mheshimiwa Mbunge ameainisha kwamba tunapeleka watumishi katika maeneo kama Buyungu, Halmashauri ya Kakonko, lakini asilimia kubwa ya hawa watumishi wamekuwa wakihama.

Kwa hiyo, alichokuwa anaainisha Mheshimiwa Mbunge ni kutaka Serikali moja, tujenge nyumba za watumishi ili watu wabaki; nafikiri kuongeza zile incentives kwa ajili ya watumishi wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya mkakati wa Serikali sasa hivi ni kuhakikisha watumishi wote wapya tunaowaajiri hawaruhusiwi kuhama katika maeneo yao, walau siyo chini ya miaka mitatu. Hiyo ni moja ya sehemu ya mikataba ambayo tumeiweka. Kwa hiyo, tutaendelea kuboresha mazingira kwa kutenga fedha ili kujenga nyumba za watumishi na kuongeza mahitaji mengine ambayo wanayahitaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili la kwenda Kakonko, niko tayari, hiyo nguvu ninayo na uwezo ninao na tuko tayari kwa ajili ya kuwatumikia. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Afya wa Kada mbalimbali katika Wilaya ya Kakonko?

Supplementary Question 2

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imefanya kazi nzuri ya kutuletea fedha za kujenga vituo vya afya na hospitali za Halmashauri: Je, katika Kituo cha Afya cha Lyamkena na Hospitali iliyoko Mlowa katika Mji wa Makambako, inafanya kazi na inahudumia wagonjwa asubuhi mpaka jioni; ni lini Serikali italeta watumishi ili kiweze kuhudumia masaa 24? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ambacho ameomba tu ni watumishi na katika jibu la msingi nililolijibu awali ni kwamba Serikali inatarajia kuajiri na tangazo la ajira litatolewa na Waziri wa Nchi na nafikiri inawezekana ikawa kabla ya wiki ijayo. Mara atakapolitoa, ajira zitakavyoombwa, sehemu ya watumishi tutakaowaajiri, baadhi tutawapeleka katika eneo hilo ili kuweza kusaidia. Ahsante.

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Afya wa Kada mbalimbali katika Wilaya ya Kakonko?

Supplementary Question 3

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba niulize swali dogo la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itapeleka mtaalam wa meno katika Hospitali ya Somanda Wilaya ya Bariadi kwa kuwa aliyekuwepo amestaafu? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sabu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, anachohitaji ni mtaalam wa meno na ninaamini tunapokuwa tunaajiri, tunazingatia maeneo yenye upungufu. Kwa hiyo, ninaamini pamoja na eneo analolitaja, litakuwa katika hizo sehemu za ajira ambazo zitatangazwa. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Afya wa Kada mbalimbali katika Wilaya ya Kakonko?

Supplementary Question 4

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na pongezi kubwa kwa Serikari kwa ujenzi wa vituo vya afya unaoendelea sasa, vipo vituo vya afya ambavyo vimejengwa kipindi cha nyumba lakini mpaka sasa havina watumishi wa kada ya afya wa kutosha: -

Je, ni lini sasa Serikali itapeleka watumishi hao ili wananchi wapate huduma inayostahili? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kyombo, Mbunge wa Nkenge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nilijibu swali hili kama ulivyoelekeza. Tunatambua kwamba kuna changamoto ya uhaba wa watumishi katika kada ya Afya.

Moja ya mikakati ni pamoja na Serikali kuajiri. Katika mwaka wa huu wa fedha 2021/2022 Serikali inatarajia kuajiri. Waziri wa Nchi atakapokuwa ametangaza ajira hizi, maana yake tutaainisha na kupeleka maeneo yale ambayo yana uhaba mkubwa wa watumishi kuhakikisha kwamba huduma za afya huduma za Afya zinaanza. Kwa hiyo, hilo ndilo jibu la msingi na niwahakikishie tu Waheshimiwa Wabunge kwamba tutazingatia maeneo yote ambayo hayana watumishi. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Afya wa Kada mbalimbali katika Wilaya ya Kakonko?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Waziri kwa kuwa muwazi na kuwa mtu mzuri. Alitembelea Vunjo baada ya kuahidi hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni hivi, je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kuinua hadhi ya OPD Himo kuwa Kituo cha Afya kwa kutekeleza majengo matatu yanayostahili pale, pamoja na watumishi wanaohitajika?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Kimei, Mbunge wa Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ambacho anahitaji tu ni kwamba kwenye eneo hilo la Himo tupandishe hadhi, tuongeze watumishi, tujenge jengo la OPD na anachotaka kufahamu tu, ni lini sasa ile huduma ambayo ameikusudia Mheshimiwa Mbunge itatekelezeka?

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba Serikali imelipokea na tutalifanyia kazi kwa sababu Serikali ya Awamu ya Sita moja ya ajenda yake kubwa kabisa ni kuhakikisha tunaboresha huduma za afya nchini. Ahsante sana.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naomba nimpongeze sana Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Nimesikiliza hapa maswali kwenye Ofisi ya Rais, TAMISEMI takribani Wabunge wengi ambao wamekuwa wakiuliza maswali ya nyongeza wamekuwa na hofu ya uhaba wa watumishi na hasa kwenye sekta ya elimu na sekta ya afya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasimama hapa kwa heshima kubwa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, naomba niwaarifu Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Rais na Serikali yake wametambua tatizo hili la uhaba wa watumishi na hasa kwenye miradi ya sekta ya afya na sekta ya elimu. Hivyo basi, Mheshimiwa Rais ametoa kibali. Ahadi ya Serikali kwa mwaka huu wa fedha ilikuwa tuajiri watumishi 44,000; tayari Serikali ilishaajiri watumishi wapya na wa ajira mbadala 12,000. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwathibitishie Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Rais ameridhia na wiki ijayo nitatoa tangazo rasmi la ajira 32,000 na utaratibu wa ajira hizo na mgawanyo wake katika sekta ambazo zinaongoza kwa uhaba wa watumishi, maelezo yote nitayatoa wiki ijayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge, Serikali ya Awamu ya Sita inajali tatizo la uhaba wa watumishi nchini. (Makofi)