Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 13 2022-04-06

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka Watumishi wa Afya wa Kada mbalimbali katika Wilaya ya Kakonko?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Jimbo la Buyungu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2020/2021 Serikali iliajiri Watumishi wa kada za afya 2,726 ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko ilipelekewa watumishi 24 waliopangwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022 imepanga kuajiri watumishi wa kada mbalimbali za afya kwa ajili ya kuboresha hali ya utoaji huduma za afya nchini kote ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na wadau itaendelea na mpango wa kuajiri watumishi wa kada za afya kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. (Makofi)