Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali wa kuboresha usafiri wa reli ya Kigoma-Dar es Salaam ambao unafanya safari mara mbili kwa wiki?

Supplementary Question 1

MHE.KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Spika, kwanza naipongeza Serikali kwa hatua ambayo inachukua, hata hivyo ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza. La kwanza, uzoefu unaonyesha kwamba wanaponunua mabehewa mapya wanayapeleka katika route nyingine na route hizo mabehewa yaliyochakaa huko ndiyo wanayaunga kwenye route ya Kigoma. Sasa nataka commitment ya Serikali kwamba mabehewa haya 22 mapya yatakayokuja yatawekwa kwenye route hii?

Mheshimiwa Spika, la pili, kwa sababu mabehewa yanayokarabatiwa ni 39 na mapya ni 22 jumla ni mabehewa 59 na bado ni machache na ukizingatia kwamba Serikali ina mkakati wa kuhama kutoka kwenye narrow gauge kwenda standard gauge; je, Wizara ina mpango wa kukarabati mabehewa zaidi ili yaweze kutumika badala ya kununua mapya ambayo tukianza standard gauge tutayaacha?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shaban Ng’enda, Mbunge wa Kigoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza anataka kujua commitment ya Serikali kwamba mabehewa hayo 22 mapya je, yatakwenda Kigoma. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mabehewa haya 22 yenye thamani ya zaidi ya dola za Kimarekani milioni 14.9 yatakwenda Kigoma na namwalika siku yatakapofika nchini Septemba mwaka huu awe sehemu ya kuyapokea haya mabehewa.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, anasema reli inayotengenezwa ni ya standard gauge na tuliyonayo ni ya meter gauge tunaonaje kwamba hizi reli ziweze kufanya kazi kwa pamoja, lakini pili ziendane na uhitaji wa mabehewa tuliyonayo. Turn worksheet ya Mheshimiwa Mbunge kwamba reli ya sasa ya meter gauge ina meter moja na standard gauge ina meter 1.475 kwa namna yoyote ile reli tuliyonayo tutaendelea kuitumia hadi hapo itakapokuja kukamilika ya standard gauge. Hata ikikamilika, lakini bado hii pia tutaendelea kuitumia. Kwa maana hiyo bado tutaendelea kukarabati mabehewa tuliyonayo kwa sababu tender ya kutangaza kutoka Tabora kwenda Kigoma ili ijengwe standard gauge bado itachukua muda. Kwa hiyo bado tutaendelea kutumia ya meter gauge. (Makofi)

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali wa kuboresha usafiri wa reli ya Kigoma-Dar es Salaam ambao unafanya safari mara mbili kwa wiki?

Supplementary Question 2

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Reli ya Kaliua – Mpanda ni mbovu na ndiyo maana inasababisha mabehewa nayo kuwa mabovu Serikali inasema nini katika hili?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Mpanda Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli reli ya kutoka Kaliua – Mpanda ina changamoto, lakini kama Serikali kupitia shirika letu la reli nchini kila mwaka tumekuwa tukitenga fedha kwa ajili ya kukarabati reli hii. Pia habari njema ni kwamba Mheshimiwa Rais ameridhia kwamba kitangazwe kipande hiki cha Kaliua - Mpanda mpaka Karemi ili kiwe standard gauge. (Makofi)