Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 9 2022-04-05

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: -

Je, nini mpango wa Serikali wa kuboresha usafiri wa reli ya Kigoma-Dar es Salaam ambao unafanya safari mara mbili kwa wiki?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kilumbe Shaban Ng’enda, Mbunge wa Kigoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Shirika la Reli Tanzania (TRC) linafanya safari mbili kwa wiki kutoka Dar es Salaam kwenda Kigoma na hii ni kutokana na uhaba wa mabehewa ya abiria. Ili kuondokana na changamoto ya upungufu wa mabehewa, Shirika lilianza taratibu za kukarabati mabehewa 37 ambapo mwezi Juni, 2021 ulisainiwa mkataba wa ununuzi wa vipuri kwa ajili ya ukarabati wa mabehewa hayo. Vipuri hivyo vinatarajiwa kuingia nchini mwishoni mwa mwezi Aprili, kwa maana ya mwaka 2022 na mara vitakapowasili kazi ya ukarabati itaanza. Kazi hiyo ya ukarabati inatarajiwa kufanyika kwa muda wa miezi nane hadi Desemba, 2022 kupitia mafundi wetu wa ndani.

Aidha, Shirika limesaini Mkataba wa ununuzi wa mabehewa mapya ya abiria 22. Mabehewa hayo yanatarajiwa kuingia nchini mwezi Septemba, 2022.

Mheshimiwa Spika, naomba kuchukua fursa hii kumwomba Mheshimiwa Kilumbe Shaban Ng’enda pamoja na wananchi wa Kigoma kuwa na subira wakati Serikali inaendelea na zoezi la ukarabati na ununuzi wa mabehewa ya abiria. Baada ya utekelezaji wa kazi hizo, idadi ya safari za treni kutoka Dar es Salaam hadi Kigoma zitaongezeka kutoka safari mbili hadi nne kwa wiki.