Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuingiza Wananchi wengi zaidi kwenye Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nimpongeze Waziri kwa majibu yake mazuri ambayo yanatia moyo na vile vile niwapongeze Mawaziri wangu hawa wa Utumishi kwa jinsi wanavyofanya kazi, wanafanya kazi sana katika hasa masuala haya ya TASAF wanafanya kazi kutoka hapa Tanzania Bara mpaka Zanzibar.

Mheshimiwa Spika, nina swali moja tu la nyongeza, pamoja na jitihada hizo Serikali inasema nini katika kuhakikisha wanaofikiwa ni walengwa zaidi? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI
WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumeboresha kwanza mifumo ya namna ya kuweza kuwapata walengwa na tumeenda kidigitali zaidi, wale waandikishaji wanatumia teknolojia, kwa kutumia tablets (vishikwambi), kuwaingiza walengwa katika mfumo wa TASAF.

Mheshimiwa Spika, vile vile kuna mfumo mwingine ambao umeongezwa wa malalamiko kwa wale ambao wanaona huenda walistahili kuwemo kwenye mpango wa TASAF, lakini waliachwa, basi kuna mfumo wa malalamiko na yale malalamiko yao yakiwekwa huwa yanapitiwa na wataalam wa TASAF na kuweza kuwarejea kuwahakiki tena na kuona kama wanastahili.

Mheshimiwa Spika, niseme tu kwamba mfumo uliowekwa wa namna ya kuwapata walengwa wa kaya maskini huwa hauanzii juu kwenda chini, mfumo ule unaanzia chini kwenda juu kwa maana Serikali ya Kijiji na wananchi hukutana katika mikutano ya kijiji na wanaanza kwa kutambuana wao kwamba fulani ni kaya maskini fulani si kaya maskini. Kwa hiyo, mfumo ule umeanza toka kijijini kuja mpaka juu sasa tayari Serikali imechukua hatua hizo lakini tunazidi kusisitiza wale wanaoenda kuandikisha kule kwa kushirikiana na Watendaji wetu wa Vijiji na Kata kuwa wakweli na kuhakikisha haonewi mtu katika wale wanaostahili kuingia katika mpango wa TASAF, basi waingizwe katika mpango wa TASAF nao waweze kuwa katika walengwa ambao wananufaika na mradi huu.

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuingiza Wananchi wengi zaidi kwenye Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini?

Supplementary Question 2

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, kwenye mpango huu wa kunusuru kaya maskini kulikuwa na mapendekezo ya kutoa kipaumbele kwa watu wenye ulemavu wanaokidhi vigezo. Je, ni kwa kiasi gani mapendekezo hayo yamezingatiwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI
WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Ikupa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kipaumbele kimewekwa hasa kwa watu wenye mahitaji maalum na kuangalia kwamba wanakidhi vigezo vile. Kwa sababu unakuta kuna watu wana hitaji maalum wenye ulemavu, lakini wanapopitiwa na dodoso lile wanagundulika kwamba vigezo vile vinavyotakiwa kuingia katika kaya ya walengwa hawajavifikia, lakini wengi ambao wamefikia huwa wanapewa kipaumbele na wanaingizwa katika mpango.

Mhshimiwa Spika, nimwongezee tu Mheshimiwa Mbunge, tunayo vile vile program ambayo inasaidia watu wenye ulemavu ili kuwa kwenye vikundi vya uzalishaji na wanapewa fedha kutoka Mfuko huu wa TASAF kuweza kuanzisha biashara zao, kwa hiyo tunatoa kipaumbele kwa watu wenye ulemavu.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuingiza Wananchi wengi zaidi kwenye Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru lengo la mfuko huu ni kusaidia kaya maskini lakini unakuta bado haileti tija kutokana na pesa ambazo wanatoa elfu 50, laki, mwisho tunawafanya wanakuwa tegemezi. Ni mkakati gani wa Serikali kuhakikisha unabadilisha huu mfumo na matokeo yake kwenda kuwapa mitaji ili wasiendelee tena kutegemea zile 50, 50 waweze kukidhi maisha yao moja kwa moja? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI
WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, tunatoa elimu kwa wale waratibu wetu kule chini na wao waweze kutoa elimu kwa walengwa ya namna bora ya kuweza kuzitumia fedha hizi wanazozipokea. Tukiangalia kwamba kaya hizi nyingi zilikuwa hazina uhakika wa kula yao, hazina uhakika wa milo mitatu.

Kwa hiyo kwa kuingia kwenye mpango huu kwa kupata kiwango cha fedha ambacho Mheshimiwa Bulaya amekitaja na wengine hupata zaidi, imeshawapa boost ya kutosha ya kuweza kuanza kufuga kuku, mbuzi ili kuweza kuboresha maisha yao na kuwa na uhakika wa kula kila siku.

Mheshimiwa Spika, vile vile tunawasisitiza sana wenzetu wa Serikali za Mitaa kwa maana Wakurugenzi kule kuhakikisha wanawaweka hawa walengwa katika mpango wa ile 4, 4, 2. Kwa sababu kwenye kaya hizi maskini wapo akinamama, kwenye kaya hizi maskini wapo walemavu, kwenye kaya hizi maskini wapo vijana. Kwa hiyo tunasisitiza sana kwamba hawa walengwa waliokuwepo kwenye kaya hizi kuweza kuingia katika 4:4:2 ili waweze kupata mkopo wa vikundi kuweza kuongeza kipato na kuweza kufanyabiashara mbalimbali.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuingiza Wananchi wengi zaidi kwenye Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini?

Supplementary Question 4

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa mpango huu kwa Wilaya ya Rorya kuna vijiji zaidi ya 20 na nimeshamtumia Mheshimiwa Waziri, ambavyo wengi wao wame-raise malalamiko ya kuachwa kwenye mpango wenyewe kipindi unatekelezwa. Nataka nijue nini mkakati wa Wizara kwenye vile vijiji ambavyo hasa watu wanalalamika kwamba waliachwa kipindi cha awali katika mpango wa utekelezaji wa TASAF. Nashukuru.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI
WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kama nilivyokuwa nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, naomba nimjibu Mheshimiwa Chege kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, jibu ni hivyo hivyo kwamba kaya zote ambazo zilikuwa zimeachwa na zinastahili kuingia katika mpango, awamu hii ya pili zinaingizwa zote kwenye mpango huu. Vile vile vijiji vyote ambavyo vilikuwa vimesalia havikuingia kwenye mpango huu wa TASAF, sasa vinaenda kuingia katika mpango huu wa TASAF.

Mheshimiwa Spika, sasa huenda nione ni namna gani nitakutana na Mheshimiwa Chege ili tuweze kupanga, tuone tunasaidiaje hivi vijiji 20 ambavyo anavyo jimboni kwake, kuweza kuona tunakwenda kuziona ama tunawaelekeza wenzetu wa TASAF waweze kufika katika jimbo la Mheshimiwa na kuona tunawasaidiaje walengwa hawa.