Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 1 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 4 2022-04-05

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuingiza Wananchi wengi zaidi kwenye Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwntumu Dau Haji, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Utekelezaji wa Kipindi cha Pili cha Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaendelea katika maeneo ya Mamlaka 186 ikiwa ni Halmashauri 184 za Tanzania Bara na Zanzibar. Katika kipindi hiki, idadi ya walengwa iliyobaki awali ya asilimia 30 ya Vijiji, Mitaa pamoja na Shehia 7,217 ambazo hazikufikiwa katika kipindi cha kwanza imeongezwa. Jumla ya kaya 498,091 zilizokidhi vigezo zimeandikishwa na kuingizwa kwenye mifumo ya taarifa za walengwa. Aidha, Kaya mpya na ambazo zilikuwemo kwenye Mpango, zinafanya jumla ya idadi kuu ya walengwa kuongezeka na kufikia kaya 1,279,325.