Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Kituo cha Afya Kiloleli pamoja na kupeleka Vifaa kwenye Hospitali ya Wilaya Busega?

Supplementary Question 1

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; Kituo hiki cha Afya Kiloleli kinahudumia zaidi ya Kata tatu kwa maana ya Kiloleli, Nyaruhande pamoja na Rubugu, lakini kina kituo cha afya kimoja: Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa wodi ya wanawake, watoto pamoja na wanaume ili kukidhi mahitaji ya kituo cha afya hiki?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, Waziri yuko tayari kutembelea Kituo cha Afya Kiloleli ili kuona mahitaji ya wananchi hawa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Jimbo la Busega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, alichoomba Mheshimiwa Mbunge ni kwamba, pamoja na kwamba kituo hiki cha afya kinafanya kazi, ameomba tu tuongeze fedha kwa ajili ya wodi tatu ili kuhakikisha kwamba kiwe full kwenye matumizi yake.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa sababu sasa hivi tumekuwa tukipata fedha karibu kila mwezi na zile fedha tumekuwa tukizielekeza kule, kwa hiyo, fedha nyingine tutatenga kwa ajili ya kuhakikisha tunapata wodi tatu katika kituo hiki ili kiwe full katika matumizi yake.

Mheshimiwa Spika, la pili, ameomba kwenda kutembelea. Najua ni rafiki yangu na anaelewa kwamba nikitembelea pale atapata mambo mengi na mema. Nimhakikishie tu kwamba tutakwenda pamoja, tutatafuta moja ya weekend tukiwa katika kipindi cha Bunge hili refu tufike ili tuone hizo kero ambazo amezizungumza. Ahsante sana.

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Kituo cha Afya Kiloleli pamoja na kupeleka Vifaa kwenye Hospitali ya Wilaya Busega?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, nini mpango wa Serikali kuhusu kuongeza vifaa tiba kwenye Kituo cha Afya Nyamwaga, Wilaya ya Tarime ili kipandishwe hadhi kiwe Hospitali ya Wilaya, ikizingatiwa Wilaya ya Tarime ina uhitaji mkubwa kutokana na jiografia ilivyo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Agnes Marwa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ambacho Mheshimiwa Mbunge ameomba tu hapa ni kwamba, lini Serikali tutaongeza fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba katika Kituo cha Afya cha Nyamwaga ili kiweze kuendelea kuhudumia watu? Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali imesikia ombi lake na tutafanya tathmini tuone ni vitu vingapi ambavyo vinahitajika kwa wakati huu ili viweze kutoa ile huduma stahiki. Ahsante sana.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Kituo cha Afya Kiloleli pamoja na kupeleka Vifaa kwenye Hospitali ya Wilaya Busega?

Supplementary Question 3

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI aliyetangulia, Mheshimiwa Ummy, alipita Jimbo la Kalenga na akaahidi kunipa shilingi milioni 300 katika Kituo cha Magulirwa pamoja na cha Kibena: Je, ni lini hizo fedha zitakuja ili tuweze kumalizia vituo hivi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Jackson Kiswaga, Mbunge wa Kalenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ambacho amekiainisha hapa Mheshimiwa Mbunge ni kwamba, Mheshimiwa Waziri alienda akatoa commitment ya kupeleka fedha. Nasi tuna mpango wetu pale Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwamba ahadi zote za viongozi zipo katika mipango yetu. Kwa hiyo, litakapokuwa limekamilika hili, basi hizi fedha ambazo zimeahidiwa zitapelekwa katika hayo maeneo ambayo Mheshimiwa Waziri aliahidi. Ahsante sana.

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Kituo cha Afya Kiloleli pamoja na kupeleka Vifaa kwenye Hospitali ya Wilaya Busega?

Supplementary Question 4

MHE. ANNA K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Naomba kuuliza Serikali, Kata ya Vunta katika Jimbo langu la Same Mashariki lina kituo cha afya ambacho kina jengo moja tu. Sasa Serikali naomba niulize kwamba, mnafanya mpango gani wa kurekebisha ili kiwe kituo cha afya hasa chenye majengo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, Mbunge wa Same Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli hayo maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge anaeleza, mimi mwenyewe nimefika katika Tarafa ya Mamba Vunta kule, ni milimani kweli kweli; na nimeona changamoto ambayo Mheshimiwa Mbunge ameiainisha. Nami nikiwa kule niliwaahidi wananchi kupitia maombi ya Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali kutokana na mahitaji na umbali wa eneo lile tutapeleka kituo cha afya katika Tarafa ile nyingine. Kwa hiyo, ile ahadi ambayo nimeizungumza ipo katika bajeti inayokuja. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge ondoa shaka katika hilo. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Kituo cha Afya Kiloleli pamoja na kupeleka Vifaa kwenye Hospitali ya Wilaya Busega?

Supplementary Question 5

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii. Serikali ilijenga Kituo cha Afya Mtakanini na kumaliza mwaka 2020, lakini mpaka leo hakina vifaatiba hasa katika majengo ya upasuaji: Je, ni lini Serikali itanunua vifaatiba katika Kituo cha Afya cha Mtakanini? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika,
ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, vile vituo tulivyoanza navyo, kuna vituo vya mwanzo ambavyo tulitoa fedha na ambavyo vimeshakamilika, tumeshaanza kupeleka fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba ili vile vituo vianze kukamilika; na tutapeleka hivyo katika awamu ya pili. Kwa hiyo, nimhakikishie tu kwamba, lipo katika mpango na watapata hivi karibuni. Nimhakikishie kwamba hicho kituo cha afya na chenyewe kinaanza kufanya kazi kwa sababu nafahamu kwamba hii ni commitment ya Serikali na fedha ipo na tumekuwa tukifanya hivyo. Ahsante.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Kituo cha Afya Kiloleli pamoja na kupeleka Vifaa kwenye Hospitali ya Wilaya Busega?

Supplementary Question 6

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa changamoto iliyoko Busega inafanana kabisa na changamoto iliyoko Wilaya ya Kiteto: Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za ujenzi wa vituo vya afya katika Tarafa zifuatazo: Tarafa ya Dosidosi, Tarafa ya Makame pamoja na Tarafa ya Kibaya? Ahsante sana kwa kunipa nafasi.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asia Halamga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, yeye ameomba kwamba, vituo vitatu katika Tarafa tatu ambazo ameziainisha hapo.

Mheshimiwa Spika, unatambua kabisa kwamba Serikali ya Awamu ya Sita, moja ya kazi kubwa ambayo tumeifanya sasa hivi ni kuhakikisha Tarafa zote ambazo hazikuwa na vituo vya afya, tumepeleka fedha na ujenzi unaanza.

Kwa hiyo, miongoni mwa maeneo ambayo ameyataja, zipo baadhi ya Kata, sehemu ya hizi Tarafa alizozitaja, tumepeleka vituo vya afya na ujenzi unaendelea. Kwa hiyo, nimwondoe shaka kwamba hivyo vituo vitakamilika na tutaleta na vifaa tiba ili kuhakikisha wale wananchi wanapata huduma ya afya kama ambavyo Serikali imekusudia. Ahsante.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Kituo cha Afya Kiloleli pamoja na kupeleka Vifaa kwenye Hospitali ya Wilaya Busega?

Supplementary Question 7

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante. Halmashauri ya Mbulu Vijijini haina vifaatiba. Je, Serikali ina mpango gani kuleta vifaatiba kwenye Halmashauri hii?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nilijibu kwa Wabunge wa awali kuhusu vifaatiba ni kwamba, sasa hivi moja ya jukumu kubwa ambalo tunalifanya sasa Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ni kupeleka fedha kwenye hospitali na vituo vya afya ambavyo vimekamilika kwa ajili ya kununua vifaatiba; na hilo limekuwa likifanyika. Kwa hiyo, hata yeye katika Halmashauri yake najua kwamba akiwasiliana nao kule kuna fedha nyingine tumepeleka Machi, mwaka huu kuhakikikisha wananchi wale wanapata vifaatiba. Kwa hiyo, hilo ndiyo jibu la Serikali kwa ujumla katika maeneo yote ambayo yanahitaji vifaatiba. Ahsante sana.

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Kituo cha Afya Kiloleli pamoja na kupeleka Vifaa kwenye Hospitali ya Wilaya Busega?

Supplementary Question 8

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa na mimi nafasi: Kituo cha afya cha Lupa Tingatinga ndiyo kituo cha afya kikubwa zaidi kwenye Tarafa ya Kipembawe, lakini kituo hiki hakina wodi yoyote kwenye Tarafa hii. Je, ni lini sasa Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kujenga wodi kwenye Kituo cha Afya cha Lupa Tingatinga?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Masache Njelu Kasaka, Mbunge wa Lupa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge ameainisha hapa kwamba, kwenye Kituo cha Afya cha Lupa Tingatinga, na bahati nzuri hili eneo nalifahamu na changamoto zake nazijua, ninajua kazi ambayo Mheshimiwa Mbunge amekuwa akipambania pale ni wananchi wake kupata wodi. Nimhakikishie tu kwamba, tutaliweka katika mipango ya Serikali ili tuhakikishe wanapata wodi na hicho kituo kiendelee kutoa huduma. Ahsante sana.

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Kituo cha Afya Kiloleli pamoja na kupeleka Vifaa kwenye Hospitali ya Wilaya Busega?

Supplementary Question 9

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kibiti kwenye Kata ya Bungu tuna ahadi ya Mheshimiwa Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kutupa shilingi milioni 250 kumalizia kituo cha afya. Ni lini Serikali italeta fedha hizo ili tuweze kumalizia kile kituo cha afya?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika,
ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Twaha Mpembenwe, Mbunge wa Kibiti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kwamba, tulishatoa fedha awamu ya kwanza shilingi milioni 250 katika vituo ambavyo asilimia kubwa ya Wabunge walipata, ikiwemo katika Jimbo la Kibiti ambalo Mheshimiwa Mbunge ameainisha. Nimhakikishie tu kwamba kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha tutatoa fedha nyingine shilingi milioni 250; na katika awamu ya kwanza tayari vituo vya afya 100 tumeshapeleka shilingi milioni 250 kumalizia ile shilingi milioni 500 na bado vituo vya afya kama 123 ambavyo tutamalizia kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha watapata hiyo fedha, shilingi milioni 250 ili waweze kumaliza vyote. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Kituo cha Afya Kiloleli pamoja na kupeleka Vifaa kwenye Hospitali ya Wilaya Busega?

Supplementary Question 10

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Zahanati ya Mabwepande imechakaa na kusababisha wananchi na watumishi kuhudumiwa nje ya kituo chini ya mti: Je, ni lini Serikali itaenda kukarabati zahanati hiyo au kujenga kituo cha afya ili wananchi wa Mabwepande waweze kupata huduma? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felista Njau, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja ya mpango ambao sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tulikaa na Halmashauri zenye mapato makubwa ikiwemo Halmashauri ya Kinondoni, Jiji la Dar es Salaam pamoja na Ilala na Temeke. Tuliwaambia kwamba, kwa sababu maeneo yenu yana fedha kubwa, basi mhakikishe mnatenga fedha kwa ajili ya ukarabati. Kwa hiyo, kupitia swali hili ambalo Mheshimiwa Mbunge ameainisha hapa, nimwagize Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kinondoni kuhakikisha kwamba anapeleka fedha kwa ajili ya ukarabati wa kituo cha afya cha Mabwepande. Ahsante sana.