Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 3 2022-04-05

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Kituo cha Afya Kiloleli pamoja na kupeleka Vifaa kwenye Hospitali ya Wilaya Busega?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Simon Songe, Mbunge wa Jimbo la Busega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya Kiloleli kilipandishwa hadhi kutoka Zahanati kuwa Kituo cha Afya mwaka 2016. Serikali imeendelea kuboresha miundombinu ya Kituo hicho ambapo jumla ya shilingi milioni 57 zilipelekwa katika mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya kujenga Wodi ya Wazazi na ujenzi wa Jengo la stoo ya dawa. Aidha, katika mwaka wa fedha 2021/2022 shilingi milioni 90 zimepelekwa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya watumishi, kwa maana ya three in one, ujenzi ambao upo katika hatua ya msingi. Mpango wa Serikali ni kuendelea kutenga fedha kwa awamu.

Mheshimiwa Spika, Serikali imetenga shilingi milioni 500 katika mwaka wa fedha 2021/2022 kwa ajili ya unununuzi wa vifaa tiba kupitia Bohari Kuu ya Dawa. Tayari baadhi ya vifaa tiba vimeshapelekwa kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Busega. Ahsante sana.