Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA K.n.y. MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Ivuna hadi Chole ili kurahisisha mawasiliano kati ya Wilaya ya Momba na Songwe?

Supplementary Question 1

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Changamoto iliyopo Mkoa wa Songwe inafanana kabisa na changamoto iliyopo Mkoa wa Dodoma katika Wilaya ya Chamwino na Wilaya ya Chemba.

Ni lini Serikali itajenga barabara ya kutokea Itiso, Zajirwa mpaka Kimaha kwa maana ya Kata ya Kimaha kuunganisha na Wilaya ya Chemba?

Pili, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutokea Kimaha – Soya – Msada mpaka Wilaya ya Kondoa? Ninakushukuru. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kunti Majala, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge ameainisha hapa hizi barabara ikiwemo Itiso – Kimaha na nyingine Kimaha – Soya na maeneo yote ambayo ameyaainisha kwamba, anataka kujua tu commitment ya Serikali ni lini itajenga barabara hizo.

Mheshimiwa Spika, ninaamini katika bajeti ya fedha ya mwaka unaokuja ziko sehemu za hizi barabara alizoziainisha tumezitengea fedha na nyingine tutaendelea kutafuta fedha ili kuhakikisha barabara hizi zote zinapitika kwa wakati wote. Kwa hiyo, hilo ndio jibu la Serikali. Ahsante.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA K.n.y. MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Ivuna hadi Chole ili kurahisisha mawasiliano kati ya Wilaya ya Momba na Songwe?

Supplementary Question 2

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali kuhusiana na barabara hiyo, ombi langu ni kwamba, Serikali haioni haja katika kipindi ambacho tunasubiri matengenezo ya hiyo barabara tupate daraja la dharura ambalo limefanya kusiwe na mawasiliano kabisa ya wananchi hawa? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Condester Sichalwe, Mbunge wa Jimbo la Momba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja, ni kwamba, katika jibu letu tumeshaweka commitment ya kutenga fedha shilingi milioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo. Bahati nzuri mwaka wa fedha huu unaoanza, ambacho naweza nikamhakikishia Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Momba ni kwamba, daraja hilo litajengwa katika mwaka wa fedha unaokuja, kabla ya msimu wa mvua kuanza. Kwa hiyo, hiyo ndio commitment ya Serikali. Ahsante. (Makofi)

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA K.n.y. MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Ivuna hadi Chole ili kurahisisha mawasiliano kati ya Wilaya ya Momba na Songwe?

Supplementary Question 3

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Barabara ya kutoka Iringa Mjini kwenda Kilolo ambayo ilikuwa ni kilometa 33, lakini inapita Jimbo la Kalenga kutoka Ipogolo kwenda Kilolo, lini itajengwa kwa sababu imekuwa ni muda mrefu haijajengwa? Ahsante. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika,
ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge anahitaji tu commitment ya Serikali ya ujenzi wa barabara kilometa 33 kutokea Iringa kwenda Kilolo ambayo inapitia Kalenga ambayo muda mrefu haijajengewa. Ni kwamba barabara hii tumekuwa tukiitengea fedha za matengenezo; na kwa sababu, Serikali inazingatia umuhimu wa hayo maeneo, na ninafahamu katika mwaka unaokuja kuna fedha imetengwa kwa ajili ya kuhakikisha yale maeneo korofi yote yanatengenezwa. Ahsante sana.

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA K.n.y. MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Ivuna hadi Chole ili kurahisisha mawasiliano kati ya Wilaya ya Momba na Songwe?

Supplementary Question 4

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kumwuliza Mheshimiwa Waziri swali la nyongeza kwamba, hii barabara ambayo inazunguka fence ya kwa Waziri Mkuu; fence ile imepakwa rangi nyeupe, lakini ina vumbi na kipindi cha mvua ina tope. Ni lini mtajenga kwa kiwango cha lami ili kuweza kutunza ile fence nzuri inayozunguka kwa Waziri Mkuu yenye rangi nyeupe? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa Mheshimiwa Mbunge anachozungumza kwamba, hii barabara ya nyuma inayozunguka fence ya Waziri Mkuu ni ya vumbi na tumekuwa tukiitengeneza kwa kiwango cha changarawe. Kwa hiyo, sasa anahitaji commitment ya Serikali ya kujenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, kwa maelezo hayo, niwaagize TARURA Mkoa waende wakafanye tathmini ya ujenzi wa kiwango cha lami. Wakishakamilisha hiyo tathmini, basi watuletee Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutajua wapi ambapo tutatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo. Ahsante.